Saturday, October 2, 2010

Marekani yaomba msamaha kwa kuwafanyia majaribio ya Kaswende wananchi wa Guatemala

Marekani imeomba msamaha kuhusiana na kuwaambukiza kwa makusudi ugonjwa mbaya wa kaswende, wafungwa, wanawake na wagonjwa wa akili wa Guatemala katika majaribio yaliyofanywa na watafiti wa serikali ya Marekani katika miaka ya 1940. Katika jinai hiyo ililofanywa kwa lengo la kujaribu dawa mpya ya penisilini, wafungwa waliambukizwa kaswende kwa makusudi na baadaye kutibiwa kwa dawa hiyo. Hillarry Clinton Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amesema kuwa jaribio hilo lililosababisha maambukizo ya ugonjwa huo wa zinaa kati ya mwaka 1946 hadi 1948 nchini Guatemala ni kinyume cha maadili hata kama tukio hilo lilitokea miaka 64 iliyopita.
Rais Alvaro Colom wa Guatemala amelalamikia vikali jinai hiyo ya Wamarekani akisema ilisababisha maambukizo ya kaswende kwa mamia ya wananchi wa nchi hiyo na kwamba ni jinai dhidi ya binadamu. Kaswende ni ugonjwa wa zinaa unaoweza kusababisha matatizo ya moyo, upofu, matatizo ya akili na hata kifo.

2 comments:

Unknown said...

hawa Marekani wamesahau Mungu yupo?

Unknown said...

mamy are ok?
tume-miss mafunzo yako.
hope uko sawa just busy kwa maisha.