Sunday, March 29, 2009

Kutahiri kunazuia magonjwa ya zinaa


Wataalamu wa Marekani hatimaye wamesisitiza kuwa, kutahiri ni njia yenye kuzuia kwa kiasi kikubwa maambukizo ya magonjwa ya zinaa. Wamesema hayo baada ya kufanywa uchunguzi uliogundua nafasi muhimu ya kutahiri katika kupunguza maambukizo ya ugonjwa wa malengelenge wa zinaa na virusi vya HPV unaosababisha kensa ya kizazi au Human Papillomavirus. Pia kutahiri kunapunguza kwa kiasi kikubwa hatari ya kupatwa na ugonjwa wa ukimwi.
Uchunguzi kama huo pia ulifanywa nchini Uganda na kuwashirikisha wanaume 3,500 ambao walichunguzwa mahusiano yao ya kijinsia kwa kipindi cha miaka miwili. Matokeo yake yalionyesha kuwa, kutahiri kunapunguza maaambukizi ya Ukimwi, suala ambalo lilipelekea jamii ya Uganda kufanya kampeni za kutahiri nchini.
Wataalamu wa chuo kikuu cha Johns Hopkns wamegundua kwamba, kutahiri huweza kupunguza uwezekano wa kuambukizwa ugonjwa wa zinaa wa Herpes kwa asilimia 25, na kupunguza maambukizo ya virusi vya Papiloma kwa theluthi moja!
Human Papilomavirus au HVP husababisha kensa ya kizazi kwa wanawake, na mapele katika sehemu za siri au genital warts kwa wanaume na wanawake pia.
….haya shime tushajiishe kutahiri, kwa wale ambao hawatilii umuhimu suala hilo katika jamii yetu.
Tukumbuke kuwa, watu wasio na maradhi, huijenga jamii salama, basi tusisahau kulinda afya zetu!

Thursday, March 26, 2009

Kiungulia au Heartburn


Kiungulia au Heartburn kwa kimombo, ni miongoni mwa mabadiliko ya ujauzito yanayowatokea baadhi ya akina mama. Tatizo hilo huwapata baadhi ya wakinamama wakati wa ujauzito, kama mabadiliko ya kimwili ya kawaida.
Ni wazi kuwa wanawake wengi hulalamikia kiungulia wakati wa ujauzito. Kiungulia hicho kinachompata mama akiwa na mimba ni wazi kuwa, ni mojawapo ya athari za kawaida kabisa zinazosababishwa na mimba. Kwa kawaida kiungulia hicho humpata mama mjamzito baada ya kula chakula. Mama anapopatwa na kiungulia, kuhisi kuchomeka au moto katika koo au kifuani mwake. Kiungulia kinaweza kutokea wakati wowote, lakini hudhihirika zaidi katika miezi mitatu ya mwisho hadi minne ya ujauzito. Kuna baadhi ya akinamama pia ambao hupatwa na kiungulia na huhisi kama vile wana uvimbe kwenye koo au kifuani. Kivyovyote vile, kiungulia kinakera na tatizo ambalo linaweza kupunguzwa na kumpatia mama nafuu.
Sababu kadhaa au masuala tofauti yametajwa kuwa yanasababisha kiungulia kwa mama mjamzito. Mojawapo ya sababu za kimsingi zinazomsababishia mama mjamzito kiungulia hicho ni mabadiliko ya homoni. Homoni hizo khususan progesterone, hulegeza valve yaani vali za tumbo au vilango tumbo ambavyo kwa kawaida huzuia asidi ya tumboni kurudi kwenye umio au esophagus. Kwa hiyo, mamamjamzito hupatwa na kiungulia yaani huhisi kuchomeka kooni au kifuani, iwapo vali hizo zitashindwa kuizuia asidi hiyo. Njia rahisi ya kupunguza tatizo hilo, ni kwa mama kugawa mlo wake wa siku nzima katika sehemu sita. Yaani badala ya kula mara tatu kwa siku kama ilivyozoeleka, mama mjamzito agawe mlo wake wa siku katika awamu sita. Kwa njia hiyo mamamjamzito atatakiwa kula mlo wake mara sita kwa siku kidogo kidogo bila ya kupoteza virutibisho muhimu. Uyabisi wa tumbo na kiungulia pia ni mambo yanayotokea mara kwa mara wakati mimba inapokuwa na miezi sita na kuendelea. Masuala haya hutokea pale mfuko wa uzazi wa mama unaokuwa unapozidisha presha kwenye matumbo pamoja na tumbo.
Kwa kuzingatia kuwa mama mjamzito hawezi kurekebisha kiwango chake cha homoni au kuuzuia mfuko wake wa uzazi kukua, kuna njia nyepesi kabisa ambazo mama anaweza kuzifuata na kumsaidia kupunguza kero ya kiungulia na kwa wengine kukizuia kabisa. Hatua hizo ni kama zifuatazo: Kwanza mama mjamazito anashauriwa kula milo midogo midogo kadhaa kwa siku nzima, ikiwa na maana kuwa, anaweza kula mara sita badala ya mara tatu. Anapaswa kujiepusha na vyakula vyenye viungo vingi au vyenye mafuta mengi. Anashauriwa mara zote kula chakula kwa uchache saa moja labla ya kuingia kitandani wakati wa usiku. Mama mjamzito hapaswi kulala muda mfupi baada ya kula chakula, kwani kitendo hicho kinaweza kuchangia kiungulia. Hatua nyingine za kufuata ni kama vile mama mjamzito anapaswa kunywa maziwa mengi au mtindi kama ana uwezo huo iwapo kiungulia kinamsumbua mara kwa mara, ajiepushe na unywaji maji mengi wakati wa kula chakula, ambao unaweza kujaza tumbo lake na kumsababishia kiungulia. Mama mjamzito ajiepushe na unywaji wa vinywaji vyenye caffeine na avae nguo pana zisizobana kifuani. Mbali na njia hizo, mama mjamzito anashauriwa kulalia upande wake wa kulia kwa kutumia mito kadhaa huku shingo ikiwa imeinuka, inasaidia pia iwapo hatua zote hizo hazitamfaa mamamjamzito katika kukabiliana na kiungulia alichonacho, anashauriwa kumona daktari kwa ushauri zaidi. Dawa za antiacid zinazopunguza asidi kame vile zile zenye mchangiko wa aluminium, magnesium na calcium zinashauriwa kutumiwa kwa kufuata maagizo ya daktari. Mama anaweza kutumia dawa hizo zikiwa katika muundo wa vidonge au majimaji.
Na sasa tuangalie dondoo moja muhimu ifuatayo.
*** Mama mjamzito anayetaka kusafiri kwenda sehemu moja au nyingine anapaswa kufanya mambo yafuatayo: Kwanza kabisa anatakiwa kuchukua tahadhari zote. Tahadhari hizo ni kama vile kujikinga na ugonjwa wa malaria ambao huzidisha idadi ya vifo vya akinamama wajawazito. Mama mjamzito anashauriwa kutosafiri kwenye maeneo yenye malaria. Aidha mama anatakiwa kuwa makini na kula vyakula vyenye sumu wakati akisafiri. Kujiepusha huko ni kwa kuzingatia usafi wake wa vyakula wakati akiwa safarini, awe makini wakati wa ulaji vyakula. Kwa wale wanaosafiri nje ya nchi, baadhi ya mashirika ya ndege, mabasi nk. Hayaruhusu kusafiri mama mjamzito akiwa na mamba ya zaidi ya wiki 35, kwa hiyo wanapswa kumuona dakatri na kupata ushauri kabla ya kuanza safari. Mama hao pia wanashauriwa kutojishughulisha na kazi zinazoweza kumdhuru yeye pamoja na mtoto aliyetumboni kama vile kufanya kazi nzito, kubeba mizigo nk. Akiwa safarini, mama mjamzito anatakiwa kuripoti mara moja dalili au alama hatari kama vile kuvuja damu, kutokwa na tishu au mabonge ya damu, maumivu ya tumboni, kuvunjika kwa chupa, maumivu ya kichwa na kujisikia kizunguzungu ili kupatiwa huduma mara moja.
Natumaini mmefaidika na makala hii, basi msisahau kuzitunza Afya zenu.
Makala hii imetayarishwa na rafiki yangu wa karibu, Asma.
Ahsante sana shosti!

Linebeke la makala za tiba


Wadau wangu wa Kona ya Afya, natumaini mu wazima na mnaendelea kuzitunza afya zenu. Kama ni hivyo basi, kwa leo ninawaletea makala muhimu hasa kwa kina mama wajawazito. Niliahidi huko nyuma kuwa tutakuwa tukichambua baadhi ya magonjwa na masuala mbalimbali kwa undani na libeneke hilo ndio leo nalianza kwa kuzungumzia suala la Kiungulia. Stay with me!
Shally's med corner

Wednesday, March 25, 2009

Je wajua? Moyo ndio kituo cha fahamu na wala sio ubongo!


Je wajua kwamba, moyo ulioko katika kifua cha mwanadamu kupiga mara 100,000 kwa siku, husukuma galoni mbili za damu kwa dakika, galoni 100 kwa saa, kwa masaa 24 kwa siku, miezi na miaka yote manadamu anayoishi duniani.
Mfumo wa mishipa ya damu ambayo
husafirisha damu katika mwili wa binadamu ina urefu wa maili 60,000. Ukubwa huo ni mara mbili zaidi ya mzunguko wa dunia!.
Suala la kustaajabisha zaidi na unalopaswa kujua kuhusiana na kiungo hiki muhimu katika mwili wa binaadamu ni kwamba moyo huanza kupiga katika mwili wa mtoto mchanga pale anapoaumbwa tumboni, hata kabla ya ubongo haujaumbwa. Moyo huanza kupiga kabla hata ya mfumo wa fahamu wa kati kuumbwa!.
Kuna nadharia maarufu kwamba mfumo wa kati wa fahamu hudhibiti na kusimamia vitendo vyote vya mwandamu kuanzia kwenye ubongo lakini utafiti unaonyesha kwamba mfumo wa fahamu hauanizishi mapigo ya moyo.
Kiuhakika mapigo ya moyo huanza yenyewe, na kuna wanaosema kuwa bado haijafahamika mapigo ya moyo huanzishwa na nini. Wataalamu wanasema kuwa moyo ni kituo cha ufahamu (consciousness) na wala sio ubongo kama wengi tunavyodhani.
Daima ilinde afya yako!

Wednesday, March 18, 2009

Chuchu bandia kumfanya mtoto asipende kunyonyesha


Utafiti mpya uliofanya huko Uholanzi unaonyesha kuwa, watoto wachanga wanaopewa chuchu bandia katika wiki za kwanza za maisha yao huwa hawapendi kuendelea kunyonya.
Kinamama wengi hupatwa na matatizo ya kuwanyonyesha watoto wao katika wiki ya kwanza baada ya kujifungua, sababu kubwa ikiwasababishwa na njia isiyokuwa sahihi ya kunyonyesha au kushindwa kuwapakata watoto wao wakati wa kunyonyesha kutokana na sababu mbalimbali. Suala hili huwapelekea kuwapa watoto wao chuchu bandia au pacifier.
Kutumia chuchu bandia huathiri mafanikio ya suala zima la kunyonyesha.
Wanasayansi wanawashauri wakinamama waliojifungua kuwanyonyesha watoto wao na kuepuka kuwapa chuchu bandia katika wiki za kwanza baada ya kuzaliwa.
Tusisahau kuwa maziwa ya mama yana umuhimu mkubwa katika ukuaji wa mtoto na kumuepusha na magonjwa mbalimbali katika kipindi cha utoto.

Tuesday, March 17, 2009

Wasiokula nyama hawapatwi sana na saratani



Uchunguzi uliofanyika nchini Uingereza umeonyesha kuwa chakula kisichukuwa na nyama (vegetarian diet) kinaweza kusaidia kuukinga mwili na ugonjwa wa saratani. Uchunguzi huo uliowapima wanaume na wanawake 52,7000 umeonyesha kwamba, wale amabo walikuwa hawali nyama hawakupatwa na magonjwa ya saratani sana ikilinganishwa na waliokuwa wakila nyama. Kumeonekana kuwa magonjwa ya saratani hutokea kwa kiwango kidogo pia kwa wale wanaokula samaki kwa wingi ikilinganishwa na wanaokula nyama.
Hata hivyo katika uchunguzi huo aina moja ya saratani ijulikanayo kama colorectal cancer imeonekana kutokea kwa wingi kwa watu wasiokula nyama(vegeterians) kuliko kwa watu wengine. Suala hilo limeshangaza, kwani linapingana na utafiti wa huko nyumba ulioihusisha aina hiyo ya kensa na matumizi ya nyama nyekundu (red meat).
Madaktari wanashauri kuwa ni bora mtu ale matunda na mbogamboga kwa wingi kila siku ili kupunguza uwezekano wa kupatwa na saratani na magonjwa mengineyo.

Monday, March 16, 2009

Ukubwa wa shingo, (neck thickness) unaashiria hatari ya ugonjwa wa moyo


Kupima ukubwa wa shingo bila kuzingatia ukubwa wa kiuno, kunaweza kuonyesha hatari anayokabiliwa nayo mtu ya kupata ugonjwa wa moyo. Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na America Heart Association, ukubwa wa shingo unaweza kuonyesha kiwango cha mafuta kinchozunguka figo na moyo na hivyo kukadiria hatari inayomkabili mtu ya kupatwa na ugonjwa wa moyo.
Watu wenye shingo nene wanaweza kukabiliwa na magonjwa yanayohusiana na moyo, hata kama wana viuno vyembamba.
Utafiti mwingine umeonyesha kuwa, watu wa aina hii kwa kawaida huwa wana kiasi cha chini cha kolestroli nzuri yani HDL na kiasi kikubwa cha kolestroli mbaya yani LDL.
Hata hivyo ukubwa wa shingo (neck size) haujaripotiwa kuathiri kiwango cha LDL.
Wanasayansi wanasema kuwa, shingo nene inaashiria kuwa kiwango cha mafuta mwlini kiko juu, mafuta ambayo yanahusiana moja kwa moja na uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo. Lakini wamesema kuwa, kufanya mazoezi ni njia bora kabisa ya kupunguza mafuta mwilini.

Monday, March 9, 2009

Wachamungu hawapatwi na mashinikizo ya mawanzo na mfadhaiko wa fikra


Utafiti wa kisaikolojia umeonyesha kwamba, watu wanaofuata itikadi za kidini au wale wanaoamini uwepo wa mungu hawapatwi sana na mashinikizo kimawazo au mfadhaiko wa kifikra. Wasiwasi wa nafsi (anxiety) ni kama panga yenye ncha mbili ambazo zinaweza kumfanya mtu apatwe na mshituko hasa baada ya kutenda kosa na hata kujawa na woga. Utafiti huo uliochapishwa katika jarida la sayansi ya saikolojia umeonyesha kwamba, kuna tofauti muhimu kati ya ubongo wa waumini na ule wa wale wasioamini itikadi zozote za kidini wakati wanapokumbana na matatizo. Imeelezwa kuwa, sehemu ya mbele ya ubongo ambayo huratibu tabia kwa kutoa ishara wakati inapotakiwa kutoa au kudhibiti mambo, haifanyi kazi vizuri katika watu walio na imani ya Mungu. Kwa sababu hiyo basi waumini huwa hawana wasiwasi au hawahisi mashinikizo ya kifikra pale wanapofanya makosa.

Bibi Sara Obama kusaidia katika kampeni za kupambana na mbung'o


Umoja wa Afrika umetangaza leo kwamba Sara Obama, bibi yake Rais Barack Obama wa Marekani atatumia umaarufu wake kusaidia katika kampeni za kupambana na mbun'go, ambao wanasababisha ugonjwa wa Malalo. Timu ya AU iliyotembelea kijiji anochoishi bibi huyo cha Kogelo huko magharibi mwa Kenya imesema kuwa, Bi. Sara Obama mwenye umri wa miaka 78, amepatiwa dawa za kupambana na mbun'go pamoja na vifaa vya kutosha vitakavyotumika kuwatibu wanyama 3,000 ambao huweza kupata ugonjwa huo sawa na binadamu. Timu huyo imesema, Mama Sarah amefurahia wadhifa huo na kuahidi kwamba atakuwa balozi mzuri katika kampeni za kuwang'oa mbung'o kwenye eneo lake.
Inafaa kuashiria hapa kuwa nchi 37 za Kiafrika zinakabiliwa na mbu aina ya mbung'o ambao wanasababisha ugonjwa wa Malalo. Jitihada zinazofanywa na Umoja wa Afrika dhidi ya ugonjwa huo, tayari zimeshazaa matunda katika nchi za Botswana na Namibia.

Saturday, March 7, 2009

Obama kuondoa marufuku ya uchunguzi wa seli mama


Rais Baraka Obama wa Marekani anatarajiwa kuondoa marufuku katika fedha za kusaidia katika utafiti kuhusiana na seli mama au stem cell. Rais aliyepita wa Marekani, George Bush alizuia kutumiwa fedha za serikali kufadhili utafiti wa seli mama za ambriyo baada ya tarehe 9 Agosti 2001.
Wanasayansi wanasema kuwa, utafiti juu ya seli mama utapelekea ugunduzi muhimu katika tiba, lakini makundi mengi ya kidini yanapinga uchunguzi huo. Seli mama ni seli ambazo zina uweza wa kugeuka na kuwa aina yoyote ya seli za mwili wa mwanadamu, kama vile mifupa, mishipa na hata seli za fahamu.
Lakini kutumiwa seli mama zinazotokana na embriyo ya mwanadamu katika utafiti huo ni suala lililozua mjadala mkubwa na baadhi ya watu wanasema kuwa, utafiti huo ni kinyume cha maadili. Tayari baadhi ya wanasayansi katika uwanja huo wameonyesha kufurahiashwa na hatua hiyo ya Obama wakisema kuwa, uchunguzi huo utaendelea tena baada ya kusimamishwa kwa miaka 8. Hatua hiyo ya Obama ni katika kutekeleza ahadi zake alizozitoa kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Baadhi ya nchi kama vile Iran zinafanya utafiti wa seli mama na tayari zimepiga hatua zaidi ikilinganishwa na Marekani kuhusiana na suala hilo,

Thursday, March 5, 2009

LEARN HOW TO LIVE LONGER AND HEALTHIER


Many people would like to be healthy but do not know how to take
care of their health. It is important to know how to take care of
your health, because your health is your greatest wealth.
Do you want to live longer younger and healthier? If the answer is
yes then continue to read his article. In modern times most people
at the age of 1 to 25 years, are healthy and very active from 26 to
40 years they become tired, from 41 years up to the age of 80 they
become sick, and might have age related diseases such as Blood
Pressure, diabetes, gout, cancer, poor eye sight, backache and they die
at this age of 80 years.
Can this situation be changed? The answer is yes in fact any person
can live up to 100 years and above with better health, the secret
behind the healthy lifestyle is;

-NUTRITION
Your health is determined by the type of food you eat. The secret to
healthier life is to eat a lot of fresh and natural food, these
includes fruits and vegetables, the fruits and vegetables takes care
of your immunity, look of your skin, help the function of your bowels
and enable you to avoid constipation. Look for good source of
protein, such as soya beans, beans, white meat, such as fish and
chicken .Eat sugars and carbohydrates sparingly because excessive use
of sugars and carbohydrates may cause overweight problems, diabetes
and blood pressure. Avoid artificial foods polished packed foods
because their usage in long run may cause different types of
cancers, These type of foods are packed with food colors and
preservatives which have toxic effects.

-AIR
Sleep with your windows open avoid polluted air and places, lack of air causes fatigue.

-EXERCISE
Your body needs some exercise to burn some excessive fat in your
body, assist natural bowel elimination and tone cells in the body.
You can join gyms, walk, jog or use the stairs when visiting offices
with storey buildings.

-REST
Respect your body's need for rest, don't overwork yourself. Go to bed
earlier the latest time you may go to sleep is 1 hour before
midnight. Have 8 hours of sleep 8 hours of work and 8 hours of
relaxation.

-WATER
Is the internal and external cleanser, drink at least 2 glasses of
water 30 minutes before every meal. Take a warm bath because warm
water kills germs and remove unwanted fat on the body.

-YOUR ATTITUDE
Have a positive mental attitude about yourself and life in
general. LOVE YOURSELF. Don't be proud, be humble, enjoy life and live today.
Have a positive self talk such as, i am a winner, day after day i am changing for the better...etc.

-DO YOU BELIEVE IN GOD?
If you do it is o.k.
if not i cannot force you. If you believe in God Pray to your God
for success, and assistance in solving your problems. Don't worry ,be
happy.

WHAT TO AVOID

-DRUGS
If you want to be mentally healthy do not take drugs .i.e
marijuana, cocaine etc.

-SMOKING
Smoking is bad for your health because it is the major cause of
cancer of the lungs., impotence, blood pressure, and bad body smell. If
you want to know much about the effects of smoking, ask your doctor.

-ALCOHOL
Take 1 litre per day or if you fail to control your self abstain from
taking it. Excessive drinking of alcohol can cause lack of
appetite, liver failure, broken marriages, digestive disorders and
malnutrition.

-WORRY.
Don't worry and be happy. Too much worrying can make you sick, worry causes stress, insanity loss of appetite and loss of sleep.

-ANGER
Control your temper avoid unnecessary arguments, an angry person is
temporarily insane. Avoid talking when you are angry calm down and
try to talk in lower voice.

-SEXUAL DESIRES
Control your sexual desires because uncontrolled sexual desires can
cause a lot of troubles to you. You might end up in jail for rape.

Wednesday, March 4, 2009

Uchunguzi mpya umeonyesha kuwa, kuangalia TV kwa muda mrefu huleta athma kwa watoto



Watoto wenye kuangalia televisheni kwa zaidi ya masaa mawili kila siku wanakabiliwa na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa athma.
Uchunguzi huo umeonyesha kuwa, kuangalia televisheni kwa muda mrefu kunaleta uwezekano wa kupata athma uongezeke mara mbili kwa watoto.
Jinsi mfumo wa kupumua unavyofanya kazi wakati mtoto anapokaa tu bila kufanya chochote, hupelekea kutokea mabadiliko katika mapafu pamoja na magojwa mengine ya kupumua ikiwemo athma. Unene wa kupita kiasi pamoja na kutokufanya mazoezi kunakosababishwa na kuangalia muda mrefu televisheni hupelekwa kutokea hali hiyo Wataalamu wamesema kuwa, kuishi maisha ya kutokuwa na harakati yoyote katika umri mdogo hupelekea kuongezeka uwezekano wa hatari ya kupata athma ukubwani. Hivyo wamewashauri wazazi kuwashajiisha watoto wao kufuata maisha ya kawaida ya kuwa na mishughuliko na kupunguza muda wanaoutumia kuangalia TV. Wataalamu wa Uingereza wametoa taarifa hiyo baada ya kuwafanyia uchunguzi watoto 3,000 wa nchi hiyo kuanzia wale waliozaliwa mpaka walio na miaka 11.
Athma ni ugonjwa sugu ambao mara nyingi unawapata watoto ambapo hushindwa kupumua, pumzi kuwabana, kukohoa pamoja na kubwana na kifua.

Tuesday, March 3, 2009

Vyakula vyenye omega 3



Aina mbalimbali za njugu (nuts) maragwe, samaki, mafuta ya mimea kama mafuta ya zaituni ni miongoni mwa vyakula vyenye Omega 3.
Fatty acid aina ya Omega 3 ina faida nyingi mwilini ikiwepo ile ya kusaidia moyo na hata kupunguza shinikizo la damu. Wachunguzi pia wamegundua omega 3 husaidia ubongo kufanya kazi nzuri hasa kwa watoto na vile vile ina faida katika ukuaji wa kawaida wa mwili.

Monday, March 2, 2009

Kufanya kazi muda mrefu huleta usahaulifu!


Kufanya kazi kwa muda mrefu kunaongeza hatari ya kupungua kwa akili na kukumbuka mambo, suala ambalo linanapelekea kwa kiasi kikubwa mtu kupatwa na magonjwa wa usahaulifu hasa uzeeni.(dementia).
Huko nyuma uchunguzi ulionyesha kwamba kuishi maisha yasiyo mazuri, kuongezeka kwa ukosefu wa usingizi, mifadhaiko ya kimawanzo na msongo wa mambo na kutokuwa na utulivu, mambo ambayo yako katika mfululizo mzima wa kufanya kazi kwa muda mrefu, kuna uhusino na matatizo ya mishipa ya damu.
Uchunguzi uliochapishwa pia katika Jarida elimu ya Magonjwa ya mlipuko la Marekani (Epidemiology Journal of America) umeonyesha kwamba, kufanya kazi za ziada au overtime, kuna athari mbaya katika ubongo.
Kwa hivyo wale wanaofanya kazi sana wako katika hatari ya kusahau mambo lakini kwa kipindi kufupi pamoja na kushindwa kukumbuka baadhi ya maneno.
Kushindwa kufanya kazi vizuri ubongo kumeonekana kutokea zaidi kati wale wanaofanya kazi zaidi ya masaa 55 kwa wiki, suala ambalo halionekani kwa wale wanaofanya kazi kwa viwango vya kawaida.

Wanasayansi wanaamini kuwa, kufanya kazi kwa kiwango cha kawaida pamoja na kula chakula bora na kilicho kamili, maingiliano ya kijamii ya kawaida pamoja na kufanya mazoezi ya mwili na akili, kunaweza kusaidia kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya kusahau hasa uzeeni au dementia.
Haya kazi kwenu wadau, kwani hakuna anayetaka kuwasahau wajukuu zake pindi atakapozeeka. Shime tuzitunze afya zetu!