Sunday, March 29, 2009

Kutahiri kunazuia magonjwa ya zinaa


Wataalamu wa Marekani hatimaye wamesisitiza kuwa, kutahiri ni njia yenye kuzuia kwa kiasi kikubwa maambukizo ya magonjwa ya zinaa. Wamesema hayo baada ya kufanywa uchunguzi uliogundua nafasi muhimu ya kutahiri katika kupunguza maambukizo ya ugonjwa wa malengelenge wa zinaa na virusi vya HPV unaosababisha kensa ya kizazi au Human Papillomavirus. Pia kutahiri kunapunguza kwa kiasi kikubwa hatari ya kupatwa na ugonjwa wa ukimwi.
Uchunguzi kama huo pia ulifanywa nchini Uganda na kuwashirikisha wanaume 3,500 ambao walichunguzwa mahusiano yao ya kijinsia kwa kipindi cha miaka miwili. Matokeo yake yalionyesha kuwa, kutahiri kunapunguza maaambukizi ya Ukimwi, suala ambalo lilipelekea jamii ya Uganda kufanya kampeni za kutahiri nchini.
Wataalamu wa chuo kikuu cha Johns Hopkns wamegundua kwamba, kutahiri huweza kupunguza uwezekano wa kuambukizwa ugonjwa wa zinaa wa Herpes kwa asilimia 25, na kupunguza maambukizo ya virusi vya Papiloma kwa theluthi moja!
Human Papilomavirus au HVP husababisha kensa ya kizazi kwa wanawake, na mapele katika sehemu za siri au genital warts kwa wanaume na wanawake pia.
….haya shime tushajiishe kutahiri, kwa wale ambao hawatilii umuhimu suala hilo katika jamii yetu.
Tukumbuke kuwa, watu wasio na maradhi, huijenga jamii salama, basi tusisahau kulinda afya zetu!

No comments: