Tuesday, March 17, 2009

Wasiokula nyama hawapatwi sana na saratani



Uchunguzi uliofanyika nchini Uingereza umeonyesha kuwa chakula kisichukuwa na nyama (vegetarian diet) kinaweza kusaidia kuukinga mwili na ugonjwa wa saratani. Uchunguzi huo uliowapima wanaume na wanawake 52,7000 umeonyesha kwamba, wale amabo walikuwa hawali nyama hawakupatwa na magonjwa ya saratani sana ikilinganishwa na waliokuwa wakila nyama. Kumeonekana kuwa magonjwa ya saratani hutokea kwa kiwango kidogo pia kwa wale wanaokula samaki kwa wingi ikilinganishwa na wanaokula nyama.
Hata hivyo katika uchunguzi huo aina moja ya saratani ijulikanayo kama colorectal cancer imeonekana kutokea kwa wingi kwa watu wasiokula nyama(vegeterians) kuliko kwa watu wengine. Suala hilo limeshangaza, kwani linapingana na utafiti wa huko nyumba ulioihusisha aina hiyo ya kensa na matumizi ya nyama nyekundu (red meat).
Madaktari wanashauri kuwa ni bora mtu ale matunda na mbogamboga kwa wingi kila siku ili kupunguza uwezekano wa kupatwa na saratani na magonjwa mengineyo.

No comments: