Monday, March 9, 2009

Wachamungu hawapatwi na mashinikizo ya mawanzo na mfadhaiko wa fikra


Utafiti wa kisaikolojia umeonyesha kwamba, watu wanaofuata itikadi za kidini au wale wanaoamini uwepo wa mungu hawapatwi sana na mashinikizo kimawazo au mfadhaiko wa kifikra. Wasiwasi wa nafsi (anxiety) ni kama panga yenye ncha mbili ambazo zinaweza kumfanya mtu apatwe na mshituko hasa baada ya kutenda kosa na hata kujawa na woga. Utafiti huo uliochapishwa katika jarida la sayansi ya saikolojia umeonyesha kwamba, kuna tofauti muhimu kati ya ubongo wa waumini na ule wa wale wasioamini itikadi zozote za kidini wakati wanapokumbana na matatizo. Imeelezwa kuwa, sehemu ya mbele ya ubongo ambayo huratibu tabia kwa kutoa ishara wakati inapotakiwa kutoa au kudhibiti mambo, haifanyi kazi vizuri katika watu walio na imani ya Mungu. Kwa sababu hiyo basi waumini huwa hawana wasiwasi au hawahisi mashinikizo ya kifikra pale wanapofanya makosa.

No comments: