Wednesday, March 25, 2009

Je wajua? Moyo ndio kituo cha fahamu na wala sio ubongo!


Je wajua kwamba, moyo ulioko katika kifua cha mwanadamu kupiga mara 100,000 kwa siku, husukuma galoni mbili za damu kwa dakika, galoni 100 kwa saa, kwa masaa 24 kwa siku, miezi na miaka yote manadamu anayoishi duniani.
Mfumo wa mishipa ya damu ambayo
husafirisha damu katika mwili wa binadamu ina urefu wa maili 60,000. Ukubwa huo ni mara mbili zaidi ya mzunguko wa dunia!.
Suala la kustaajabisha zaidi na unalopaswa kujua kuhusiana na kiungo hiki muhimu katika mwili wa binaadamu ni kwamba moyo huanza kupiga katika mwili wa mtoto mchanga pale anapoaumbwa tumboni, hata kabla ya ubongo haujaumbwa. Moyo huanza kupiga kabla hata ya mfumo wa fahamu wa kati kuumbwa!.
Kuna nadharia maarufu kwamba mfumo wa kati wa fahamu hudhibiti na kusimamia vitendo vyote vya mwandamu kuanzia kwenye ubongo lakini utafiti unaonyesha kwamba mfumo wa fahamu hauanizishi mapigo ya moyo.
Kiuhakika mapigo ya moyo huanza yenyewe, na kuna wanaosema kuwa bado haijafahamika mapigo ya moyo huanzishwa na nini. Wataalamu wanasema kuwa moyo ni kituo cha ufahamu (consciousness) na wala sio ubongo kama wengi tunavyodhani.
Daima ilinde afya yako!

No comments: