Saturday, May 8, 2010

Kula zabibu usipatwe na ugonjwa wa moyo


Wadau msichoke na mimi kuzungumzia ugonjwa wa moyo, au nisiseme mimi, bali niseme wataalamu ambao kila siku wamekuwa wakifanya majaribio na kutuelewesha vyakula au njia zinazotuepusha na ugonjwa huu. Hii ni kwa sababu ugonjwa wa moyo kweli ni tishio duniani kote. Ni wiki iliyopita tu mfanyakazi mwenzangu ambaye nilikuwa naye kazini hadi nyakati za mwisho za kazi, siku ya pili nakuja kazini naambiwa kafariki dunia kwa mshituko wa moyo. Masikini baba wa watu!!, huku akiwa anayetegemewa na familia, akiacha mke na mtoto ameondoka kama utani tena kwa kufumba na kufumbua. Baada ya kutoka kazini alikaa juu ya kochi na kujiegemeza akisubiri atengewe msosi, lakini hapo hapo aliaga dunia. Msosi ulipotengwa na mkewe kumuamsha ale akidhani labda amepitiwa na usingizi, aliona haamki tena, na ndipo walipomkimbiza hospitalini. Huko waliambiwa ameshakufa zamaaani kutokana na mshituko wa moyo!.
Sasa hali ni hii, na hivi karibuni uchunguzi mpya umeonyesha kwamba kula zabibu au vyakula vyenye zabibu ndani yake kunapunguza shinikizo la damu, husaidia moyo kufanya kazi zake vyema na kupunguza hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo.
Kwa mujibu wa uchunguzi huo uliotolewa kenye mkutano wa Majaribio ya Bayolojia huko California, zabibi zina uwezo wa kupunguza shinikio la damu, husaidia mwili uweze kuvumilia sukari (glucose tolorance) na kupunguza kiwango cha mafuta aina ya triglycerides mwilini ambayo ni chanzo cha matatizo ya moyo.

Wataalamu wanasema zabibu pia zinaweza kupunguza uvimbe, uharibivu unaotokana na free radicals zinazozalishwa mwilini na shinikizo la moyo.
Kwa ujumla zabibi zinazuia hali inayoitwa Metabolic Syndrome suala ambalo linatokana na mada za phytochemicals zilizoko kwenye matunda hayo.
Metabolic Syndrome ni mchanganyiko wa matatizo ya kitiba ambayo yanaongeza uwezekano wa kupatwa na maradhi ya mishipa ya damu pamoja na kisukari.
Hivyo wataalamu wanatushauri tule zabibi au kuongeza zabibu katika vyakula wanavyokula kila siku, ili tujikinge na ugonjwa wa Metabolic Syndrome, ugonjwa wa moyo na kisukari aina ya pili.
Haya shime tule zabibu kwa ajili ya afya zetu!.

3 comments:

Disminder orig baby said...

mama yangu, sasa umeuwa, vile napenda zabibu! yani ukiwa msimu wa zabibu uwa haipiti saa sijala zabibu. Duh asante sana.

hakuna kuchoka we tuhabarishe na Mungu akuzidishie zaidi.

nyahinga said...

sasa nitakula zabibu mpaka nivimbewe.

babally.bligspot.com said...

Hata mm naanza