Monday, May 3, 2010

Madaktari waboronga katika upasuaji Afrika Kusini na kuhatarisha maisha


Gazeti moja nchini Afrika Kusini limefanya uchunguzi na kuripoti kuwa, madakitari wa upasuaji nchini humo wanafanya kazi isiyo ya kuridhisha na yenye kuhatarisha maisha ya wagonjwa wanaokwenda kupasuliwa. Gazeti la Sunday Independent limesema kuwa, uchunguzi wao umedhihirisha kuweko malalamiko ya waliopasuliwa, wengine wakilazimika kurudi kufanyiwa upasuaji mwingine, wanapogundua vifaa fulani vimeachwa mwilini mwao. Gazeti hilo limemnukuu msemaji wa Waziri wa Afya wa Afrika Kusini Fidel Hadebe akisema, amepokea ripoti kwa mhasiriwa mmoja aliyedai kuwa, mikasi ilibakia tumboni mwake alipofanyiwa upasuaji. Aidha uchunguzi wa gazeti hilo umeonyesha kuwa, sababu ya kushuhudiwa hali kama hizo uhaba wa matabibu nchini humo, jambo linalopelekea madaktari wachache walioko, kuboronga katika kazi zao katika juhudi zao za kuhakikishwa wanawafanyia upasuaji wagonjwa wengi.

No comments: