Saturday, January 22, 2011

Tatizo la kukosa choo watoto wadogo au kuwa na choo kigumu na jinsi ya kulitatua


Tatizo la kukosa choo watoto wadogo au kuwa na choo kigumu na jinsi ya kulitatua
Watoto wadogo hasa wale ambao bado wananyonya na ndio kwanza wamenzishwa vyakula vinginevyo zaidi ya maziwa, mara nyingi hupatwa na choo kigumu au kukosa choo kabisa hali tunayoiita kimombo, constipation. Hali hiyo huanza pale mtoto anapoachishwa maziwa ya mama na kuanza kunyweshwa maziwa ya kopo au mengineyo au pia anapoanzishwa kula vyakula vingine zaidi ya maziwa. Mara nyingi watoto wanaonyonya maziwa ya mama huwa hawasumbuliwa na tatizo hilo, bali tatizo hilo huanza kujitokeza pale wanapoanza kulishwa vyakula vingine zaidi ya maziwa ya mama. Pia mama ambaye tayari mwenyewe anasumbuliwa na tatizo la kukosa choo, huenda mwanae pia akasumbuliwa na tatizo hilo.
Mtoto mwenye tatizo la kukosa choo huwa anapata choo wa shida huku akisumbuliwa na tumbo na kupata choo kigumu. Wakati mwingine hulia wakati akipata choo huku akijiminya na kukunja uso. Muone daktari iwapo mtoto ana umri wa chini ya mwezi mmoja na hajapata choo kwa siku 4.
Iwapo mtoto wako mchanga au mdogo ana tatizo la kukosa choo au kupata choo kigumu kwanza wasiliana na daktari au mpeleke hospitalini ili upate ushari wa daktari. Pia unashauriwa kujaribu njia zifuatazo:
1. Jaribu kumpa mtoto wako maji safi na salama kuanzia mililita 60 hadi 120 kwa siku. Punguza au ongeza kiasi hicho kwa kuzingatia jinsi hali ya mwanao inavyokuwa. Ni bora maji ya mtoto yachemshwe na kufunikwa vyema.
2. Iwapo maji hayasaidii, jaribu pia kumpa juisi za matunda. Mpe mtoto wako juisi ya tufaha (apple), pea au prune iliyotengenezwa kwa kutumia maji salama na safi kila siku. Anza kwa mililita 60 hadi 120 kwa siku na punguza au ongeza kiasi hicho kwa kuzingatia jinsi hali ya mwanao inavyokuwa.
3. Jitahidi kumpa mwanao chakula chenye ufumwele au fiber. Iwapo mwanao ameanza kula vyakula vigumu, basi mpe vyakula vyenye ufumwele kuliko vyakula vyenye wanga, kama vile tumia unga wa shayiri au tunda la apple na pea lililopondwa pondwa vyema na kuwa kama uji. Epuka kumpa mtoto cereal ya mchele au uji wa mchele kama anatatizo la kukosa choo au kufunga choo.
4. Jiepushe kumpa mtoto wako vyakula vyenye wanga na sukari na vyakula vinavyotengenezwa kwa unga uliokobolewa.
5. Mpake mwanao mafuta kidogo sehemu inayotoka choo kikubwa ili kurahisisha utokaji wa kinyesi. Usitumia mafuta ya madini (mineral oil) au dawa za kulainisha choo na za kuharishwa katika kutibu tatizo hilo la kukosa choo la mtoto.
6. Kukosa choo watoto wadogo mara chache huwa kunasababishwa na magonjwa kama vile Hirschsprung ugonjwa wa kumee neva katika utumbo, au Cystic Fibrosis. Muone daktari au mpeleke mtoto wako hospitalini kama tatizo hilo la kukosa choo linaendelea hata baada ya kubadilisha aina ya chakula cha mtoto au linaambatana na dalili nyingine kama vile kutapika au mtoto kukosa utulivu na kuhangaika.
7. Kuna baadhi ya watoto wanakosa choo au kuwa na choo kigumu kutokana na kutumia maziwa ya ng’ombe. Iwapo umetumia dawa na umefuata maelekezo ya kuondoa ukosefu wa choo na hukufanikiwa. Katisha kumpa mtoto maziwa ya ng’ombe kwa siku mbili au tatu, baada ya siku hizo iwapo bado hajaacha choo badi endelea kumpa maziwa hayo, na pengine tatizo hilo halisababishwi na maziwa ya ng’ombe.
8. Mwogeshe au mweke mwanao katika beseni la maji ya uvuguvugu na hakikisha maji yanafika hadi kifuani. Mkande mtoto tumbo lake wakati akiwa majini na njia hiyo husaidia kulegeza misuli ya mwili wa mtoto, na kumsaidia kupata chook wa urahisi.
N.B Ukosefu wa choo kwa watu wazima baadhi ya wakati huandamana na magonjwa kama vile Arthritis, Appendicitis, Cataract, saratani, shinikizo la damu, Rheumatism na kadhalika lakini kwa watoto huenda tatizo hilo likawa halisababishwi na maradhi hayo.
Utafiti unaonyesha kuwa hakuna uhusiano wowote kuhusu kukosa choo mtoto na kupewa nyongeza ya chuma au Iron Supplement. Hivyo usimkatishe kumpa mwanao chuma iwapo anakosa choo. Kwani chum ni muhimu sana katika kuzuia upungufu wa damu mwilini kwa mtoto wako mdogo.

10 comments:

Paul Akwilini said...

Nashukuru kwa maelezo yako mazuri ngoja nijaribu kulifuata kwani mwanao anasumbuliwa na hilo tatizo. Pia ni kweli mama yake alikuwa anapata shida ya choo tangu akiwa na mimba hadi hivi sasa anapata nae choo kigumu na humchukua siku hadi kupata. Asante sana!

The great said...

Ahsante kwa somo nzuri amnalo halina gharama nyingi,mungu awabariki

Anonymous said...

Nashukuru sana kwa somo hili zuri maana hata mimi nina mtoto wa miezi 5 ila huwa hasumbuliwi sana na hili tatizo.

Lakini naomba kuuliza kuna watu walinambia kuwa mtoto anapopata choo kigumu au kupitisha siku zaidi ya mbili naweza kumpa CASTOR OIL...je ni sahihi au yana madhara?

Mdau...Musoma

Anonymous said...

Nilikua sijaiona hii blog mpaka leo ndio nilikua nasoma soma mara nikaikumba. Ni blog nzuri na nimependa unavyoelezea vitu.

Ninachoomba baada ya kusoma post kadhaa ni heri uweke warning hapo juu wasomaji wasome waelewe kuwa hapa ni unashauri kutokana na articles au ujuzi ila wasichukue ushauri wako kama final answer. Hiyo ndio inatakiwa kwa site zote zinazoelezea mambo ya afya. Unajua kwetu wengine kumwona Dr mpaka tuwe taabani tunapenda kuambiana tu. Utasikia mtu anasema nasikia kizunguzungu mtu mwingine anasema aah hiyo umechoka tu, huna maji mwilini kumbe una jambo kubwa zaidi.Before you know mtu androp dead. Na technologia za sasa hivi wengi wataingia tu kwenye PC na kuangalia unachoandika na kufikiria kama ndio solution. Hiyo disclaimer itasaidia kuwakumbusha watu na kuokoa maisha ya wengi..

2nd unaposema umpe mtoto maji hujaelezea ni mtoto wa umri gani. Unajua kwetu tunafanya vitu vingi bila scientific research ni ile kutokana na bibi alifanya basi na mama kafanya hivyo na mimi nitafanya. Ndio kuna vitu vingine haviitaji research alakini kuna vingine ukiangalia au kulinganisha utajua kuwa kweli ni Mungu anayetulinda au kunaambao watoto wanakufa kumbe mtu ungeelewa na kufanya vinavyotakiwa ungesaidia kuponyesha maisha ya watoto. Kwa vile mimi nilijifungua mbali, mama alikuja mwanangu alikua na miezi 7 hivyo uzazi wote nilifanya bila ya kuwa na mama yangu au hata watanzania wenzangu karibu ilibidi nitegemee madoctor, nurses na consultants tu kwa hiyo nilijifunza vitu vingi sana. Mtoto chini ya miezi sita hairuhusiwi kumpa maji. Nakumbuka nilikua naongea na mama namwambia mtoto analia mama ansema mpe maji. Sina notes zangu sasa hivi lakini nitazitafuta nikuandikieuwaonyeshe watu kuna madhara sana.

Mtoto akifungwa choo kuna Karo syrup inafanya kazi sana. Nadhani hata tanzania ipo na pia kama unavyonyesha ujue kuwa mama mwenye mtoto hana maji mwilini ndio maana mtoto hayapati maji. Ukiwa unanyonyesha baada ya kunywa soup tunazotengenezewa unatakiwa unywe maji sana. Nilikua nakunywa maji gallon moja kwa siku. Ikamaliza kabisa matatizo ya choo.

Kama mtoto anayekula chakula ndio hivyo vyakula vyenye fiber na mboga za majani zitasaidia

Jigambe Team said...

tunashukuru kwa ufahamu mnaotupa na ni vyema ili watu waijue zaidi ili kupata vitu ambavyo unavyotupa tembelea hii site ya www.tanzaniakwetu.com na www.jigambeads.com ili usajili na kuweza kupatikana kwa urahisi.

Unknown said...

nashukuru kwa somo zuri,kwani hapa nilipo nina mtoto ambae bado mdogo na wakati mwingine inatokeaga tatizo hili.asante sana na kazi njema

Anonymous said...

Mtoto wangu ana miezi 2 anapata choo Baada ya siku 2 ha

di 3 tena kwa tabu hadi analia je kunatatizo?

Unknown said...

asanteni

Anonymous said...

Nilisoma baadhi ya shuhuda kuhusu mtangazaji wa mapenzi anayeitwa DR DAWN kuhusu jinsi ambavyo amesaidia watu wengi kuwarudisha wapenzi wao wa zamani ndani ya masaa 48, kwa dhati nilikuwa nikifikiria kama hiyo ni kweli na ikiwa mwanaume huyu angeweza kusaidia kumrudisha mpenzi wangu ambaye Napenda sana. Niliamua kuwasiliana naye kwa sababu nampenda sana mpenzi wangu na tumetengana kwa miezi kadhaa. Kwa kweli nilimkumbuka sana, nimejaribu njia zingine zote kumrudisha lakini sikuweza. Niliwasiliana na DR DAWN na akaniambia kuwa ex wangu atanirudia baada ya saa 48 zijazo,
Kwa mshangao wangu Ex boyfriend wangu alirudi saa 48 haswa, shukrani kwa Dr DAWN,
Anaweza pia kukusaidia
*Tahajia ili kupata mimba.
*Tahajia ili kuungana tena.
*Tibu ugonjwa wowote.
*tahajia kwa bahati nzuri.
*Tahajia kwa ajili ya mali.
Na wengine.
Wasiliana naye kupitia: dawnacuna314@gmail.com
Whatsapp: +2349046229159

Anonymous said...

Sikuamini kuwa ningeweza kuungana tena na mpenzi wangu wa zamani, nilipatwa na kiwewe cha kusimama peke yangu bila mwili wa kusimama na kuwa nami, lakini nilipata bahati sana siku moja nilikutana na Dk DAWN, baada ya kumwambia. kuhusu hali yangu alifanya kila liwezekanalo kumuona mpenzi wangu anarudi kwangu, kiukweli baada ya kunifanyia uchawi mpenzi wangu wa zamani alirudi kwangu chini ya masaa 48, mpenzi wangu wa zamani alirudi huku akiniomba kuwa hatoniacha kamwe. tena. Miezi 3 baadaye tulioana na kuoana, ikiwa una hali sawa. Ana nguvu nyingi katika mambo yake;
* upendo
inaelezea * inaelezea kivutio
* kama unataka ex wako nyuma
*acha talaka
*kuvunja mawazo
* huponya viharusi na magonjwa yote
* uchawi wa kinga
*Ugumba na matatizo ya ujauzito
* bahati nasibu
* bahati nzuri
Wasiliana na Dk Ediomo kwenye barua pepe yake: dawnacuna314@gmail.com
Whatsapp:+2349046229159