Thursday, May 20, 2010

Chanjo ya Ndui kuzaidia kupambana na virusi vya HIV


Kutotumiwa chanjo ya ndui katika baadhi ya nchi duniani kunaaminika kuwa kumesaidia katika kueneza maambukizo ya virusi vya HIV, hasa kwa kuzingatia kuwa ugonjwa huo umeongeza sasa siku hizi. Chanjo ya ndui polepole ilianza kutotolewa katika baadhi ya nchi duniani na ugonjwa wa ndui kutokomezwa katikati mwa karne ya 20. Utafiti uliochapishwa katika jarida la BMI Immunology umeonyesha kwamba, chanjo ya ndui ilikuwa ikipunguza maambukizo ya virusi vya HIV, hasa mwanzoni ugonjwa huo ulipogunduliwa duniani. Lakini kuacha kutolewa chanjo hiyo na wataalamu wa Afya, kunaweza kuwa ndio sababu iliyopelekea ongezeko la maambukizo ya ugonjwa wa Ukimwi yaongezeke. Wataalamu waliofanya utafiti huo wanasema kwamba, kuna sababu kadhaa zilinazoweza kutolewa kuhusiana na kasi ya ongezeko la Ukimwi barani Afrika, baadhi ya sababu hizo ni vita, kurudiwa kutumiwa sindano bila kuondolewa vijidudu (unstrelizized needles) pamoja na chanjo za ndui za mwanzo ambazo zilikuwa na vijidudu. Hata hivyo, wataalamu hao wamesema kuwa, sababu zote hizo zimekanushwa au hazitoshi kuelezea sababu ya ongezeko kubwa la maambukizo ya HIV duniani hasa barani Afrika.
Chanjo ya ndui inapunguza uwezekano wa virusi vya HIV kuzaana mara kadhaa katika seli za damu. Pia chanjo hiyo huleta mabadiliko ya muda mrefu katika mfumo wa kulinda mwili, hubadilisha tafsiri ya recepta ya CCR5, ambayo iko juu ya seli za chembechembe nyeupe za damu zinazotumiwa na virusi vya ndui pamoja na HIV.
Wataalamu wanamini kwamba chanjo ya ndui itaweza kutumiwa katika kupambana na ugonjwa wa Ukimwi katika miaka ijayo ya hivi karibuni, lakini pia wamesisitiza kwamba uchunguzi zaidi unapaswa kufanywa ili kuhdibitisha zaidi suala hilo.


Ugonjwa wa ndui ni miongoni mwa magonjwa ambayo yaliitikisa dunia katika miaka ya huko nyuma. Lakini kugunduliwa chanjo ya ndui ambapo kwa kupatiwa chanjo ya ugonjwa huo mara moja mtu huweza kuwa na kinga dhidi ya ugonjwa huo kwa maisha yake yote, kulipunguza maambukizo ya ugonjwa huo na hatimaye ugonjwa huo ukang'olewa kabisa karibu katika nchi zote duniani. Ndugu mdau, kama huna uhakika kama umepatiwa chanjo ya ndui, basi angalia katika moja ya mabega yako na kama utakuta kovu dogo la duara, basi ujue kuwa una kinga ya ndui. Nawahusia wakina mama wanaowazaa watoto wao siku hizi wahakikishe kwamba wanapatiwa chanjo ya ndui, kwani kama inavyoelezwa mbali ya kumzuia mtoto wako asipate ugonjwa wa ndui maishani, pia hupunguza maambukizo ya ugonjwa wa Ukimwi. Haya tena wadau lakini wewe unafikiri ni sababu gani hasa inayopelekea ongozeko la maambukizo ya Ukimwi katika jamii zetu?..... tueleze maoni yako ili tusaiidiane katika kuifunza jamii na kupambana na ugonjwa hatari wa Ukimwi.

1 comment:

Unknown said...

lakini ilikuwa inauma.