Wednesday, May 5, 2010

Kukosa usingizi kunasababisha vifo vya mapema


Imetahadharishwa kwamba kulala usingizi wa chini ya masaa 6 kila usiku kunaweza kusababisha mtu apatwe na kifo cha mapema. Watafiti wamesema kuwa watu ambao kwa kawaida huwa wanalala masaa hayo machache wengi wao hupatwa na vifo vya mapema kwa asilimia 12 zaidi ya wale wanaolala kawaida kwa masaa 8. Vifo ambavyo hutokea katika umri wa baada ya miaka 25. Pia imeonyeshwa kwamba kulala zaidi ya masaa 9 pia kunapelekea vifo vya mapema ingawa kulala huko kunaweza kukawa na uhusiano na matatizo ya kiafya. Utafiti huo umetolewa kwa kuchunguzwa uhusiano uliopo kati ya kifo na usingizi kwa kutegemea chunguzi 16 zilizofanywa kwa kuwahusisha watu milioni 1 na nusu katika nchi za Uingereza, Marekani , Ulaya na Mashariki mwa Asia.
Profesa Francesco Cappiccio aliyeongeza utafiti huo wa chuo kikuu cha Warwick cha Uingereza anasema jamii za hivi sasa zilizoendelea zimekuwa taratibu zikipunguza muda wa kulala, na tatizo hili linawapata sana watu wanaofanya kazi masaa mengi. Amesema suala hili linaonyesha kwamba hayo yote yanatokana na mashinikizo ya kimaisha yanayowapelekea watu wafanye kazi masaa mengi na kuchukua shift nyingi za kazi. Amesema kwamba, kuporomoka kwa afya kunaambatana na kulala masaa mengi zaidi. Wataalamu wanasema kuwa, watu wanapaswa kufahamu kwa nini hasa usingizi ni suala muhimu sana kwa afya nzuri. Usingizi ni kama karatasi ya litmus inayoonyesha afya na hali ya mwili na akili ya mtu kwani usingizi unaathiriwa na magonjwa na hali mbalimbali ikiwemo msongamano wa mawazo au depression, anasema mtaalamu huyo. Inashauriwa kuwa tusilale masaa machache wala mengi bali tulala kwa masaa ya wastani ambayo ni masaa 8.

3 comments:

Unknown said...

uuh nipigie, kumbe uwa tunam-beep Mwarabu kwa kujifanya busy na kulala muda mfupi?

Shally's Med Corner said...

Lool... ni kweli babyAmore... si kwa kulala muda mfupi tu hata kwa kulala muda mrefu wa zaidi ya masaa9.

Disminder orig baby said...

asante sana kwa habari nzuri. tembea uone mamangu husema kila siku.