Friday, November 6, 2009

Namna ya Kujikinga na Homa ya Mafua ya Nguruwe….Sehemu ya Pili



1. Vaa mask za uso ili kujikinga kupata ugonjwa wa homa ya mafua ya nguruwe, hasa unapokuwa katika maeneo ya mikusanyiko.
2. Ziba pua na mdomo pale unapokohoa au kupiga chafya, ni bora ukitumia soft tissue ( karatasi za kufutia uso). Tupa katarasi hiyo baada ya kutumia mara moja tu. Ni bora ujiepushe kutumia vitambaa kwani kitambaa hutumika mara kadhaa na huweza kusadia kubeba vijidudu.
3. Ni bora ujiepushe kwenda kwenye mikusanyiko isiyo ya dharura, kwani sehemu kama hizo huweza kuwa mazingira mazuri ya kuambukizana homa ya mafua ya nguruwe.
4. Dumisha usafi, osha mikono na uso vizuri kwa sabuni mara kwa mara. Suala hilo hupunguza maambukizo ya virusi vya mafua ya nguruwe. Ni bora iwapo utatumia sabuni za kuua vijududu kama vile dettol n.k.
5. Waangalie vyema watoto kwani wao vi rahisi kupata ugonjwa huo. Wafundishe kuosha mikono kila mara na kudumisha usafi na ni bora kama watapata kinga ya ugonjwa huo.
6. Jiepushe kula hovyo, hasa vyakula vya vinavyotayarishwa nje ya nyumba, kwani huenda vikawa si salama na vikakusababishia kuambukizwa virusi vya mafua ya nguruwe.
7. Kunywa maji yaliyochemshwa.
8. Jiepushe kuwashika au kuwa karibu na nguruwe, ni bora wanyama hao watengwe ili kuepusha maambukizo ya ugonjwa huo.
9. Iwapo utajisikia dalili za mafua au dalili nyinginezo za homa ya mafua ya nguruwe ni vyema umuone haraka daktari.

Thursday, November 5, 2009

Namna ya kupima kiwango cha mafuta mwilini kwa kutumia BMI


BMI au Body Mass Index nia njia inayotumiwa kupima uzito wa mwili ukilinganishwa na urefu. Ingawa kipimo hicho hakionyeshi kiwango cha mafuta mwilini moja kwa moja lakini kinaonyesha kiwango cha unene ambao hukadiria hatari ya kupatwa magonjwa mbalimbali. Kipimo cha BMI kinatumika kwa wanawake na wanaume walio na umri wa kuanzia miaka 20 na kuendelea.
Namna ya kuhesabu BMI:
Uzito kwa kiwango cha kilogramu, gawanja kwa meta mraba ya urefu.
Kiwango cha BMI sawa au chini ya 18.5 kinaonyesha kuwa uzito wa mtu ni mdogo chini ya kiwango kinachotakiwa kiafya.
Kiwango cha BMI kikiwa sawa na 18.5 hadi 24.9 kinaonyesha kwamba uzito wa mwili ni wa kawaida na unaotakiwa.
Kiwango cha BMI kinapokuwa kati ya 25.0 na 29.9 kinaonyesha kuwa mtu ana uzito mkubwa.
Lakini kiwango cha BMI kinapokuwa 30 na kuendelea inaonyeshea kuwa uzito wa mtu ni mkubwa mno au ana obesity.
Mbali na BMI vilevile mzunguko wa kiuno au (waist size) unaozidi nchi 40 kwa wanaume na wanawake nchi 35, unaonyesha kuwa mtu yuko katika hatari ya kupata matatizo ya kiafya kama vile kisukari, shinikizo la damu pamoja na magonjwa ya moyo.

Monday, November 2, 2009

Ijue Homa ya Mafua ya Nguruwe (Swine Flu) ….sehemu ya kwanza


Homa ya mafua ya nguruwe inayojulikana kiingereza kama “Swine flue” ni ugonjwa unatokana na moja ya aina mbalimbali za virusi vya mafua ya influenza ya nguruwe au SIV. SIV au Swine Influenza Virus ni aina yoyote ya mafua ya influenza yanayotokana na virusi vinavyotokana na nguruwe. Virusi hivyo vinaweza kwa H1N1, H1N2, H3N1, H3N2 NA H2N3. Ugonjwa wa homa ya mafua ya nguruwe ni ugonjwa wa kawaida kwa nguruwe duniani kote. Maambukizo ya ugonjwa ya virusi hivyo kutoka kwa nguruwe kwenda kwa binaadamu hayatokeo kila mara. Lakini iwapo maambukizo ya binaadamu yatatokea husababisha homa ya mafua ya nguruwe kwa binaadamu pia. Watu ambao wako karibu na nguruwe wako kwenye hatari kubwa zaidi ya kuambukizwa homa ya mafua ya nguruwe, kama vile wafugaji nguruwe na wanaojishughulisha na wanyama hao.
Wataalamu wanasema kwamba mfumuko wa homa ya mafua ya nguruwe mwaka huu wa 2009, ambapo ilianzia nchini Mexico, umesababishwa zaidi na virusi vya H1N1, kwani ndio aina ya virusi ambavyo humpata zaidi mwanadamu. Ugonjwa huo kwa hivi sasa umeenea sana katika nchi nyingi duniani na Shirika la Afya Duniani WHO limeutangaza kuwa janga la kimataifa. Watu wengi wameambukizwa homa ya mafua ya nguruwe katika nchi nyingi duniani huku, ikikadiriwa kuwa karibu watu 700 hufariki dunia kila wiki kutokana na homa ya mafua ya nguruwe duniani kote. Kwa kuzingatia hayo Kona ya Afya imeona kuna ulazima wa kuzijua dalili za ugonjwa huo na kuelezea namna ya kujiepusha au kukabiliana na ugonjwa huo. Kumbuka kuwa hivi sasa ambapo nchi nyingi zinaingia katika majira ya badiri ambapo mfumuko wa magonjwa ya kifua na mafua huongezeka, hatari ya kupatwa na ugonjwa huo ni kubwa zaidi. Si lazima uwe karibu na nguruwe au unafuga na kula nguruwe ndio ufikiri unaweza kupatwa na ugonjwa huo, ukweli ni kuwa maambukizo ya homa ya mafua ya nguruwe kwa sasa ni kati ya mtu na mtu, au kwa Kiswahili kingine toka binadamu kwenda kwa binaadamu mwingine, hiyo inamanisha kuwa, sote tuko hatarini.
Dalili za homa ya mafua ya nguruwe
Kwa kawaida dalili za ugonjwa huu huwa sawa na ugonjwa wa kawaida wa mafua. Lakini pia kuwa baadhi ya watu huonyesha dalili mbaya zaidi au zinazotofautiana na mafua ya kawaida.
Iwapo mgonjwa atakuwa na homa kali zaidi ya sentigredi 30 au 100/F pamoja na moja ya dalili zifutazo, anaweza akawa amepatwa na homa ya mafua ya nguruwe na ni boda umuone daktari.
1. Maumivu ya mwili.
2. Kuumwa kichwa.
3. Mafua.
4. Mauvimu ya koo.
5. Kushindwa kupumua na kikohozi.
6. Kukosa hamu ya kula.
7. Mwili kuchoka sana kinyume cha kawaida.
8. Kuharisha na kutapika.
Ingawa ugonjwa wa homa ya mafua ya nguruwe unaweza kuwapata watu wote lakini watu wafuatao wanakabiliwa na hatari zaidi ya kupatwa na ugonjwa huo:
 Kina mama waja wazito.
 Watu wenye magonjwa ya muda mrefu ambayo yamepelekea miili yao kuwa dhaifu kama vile kensa, magonjwa ya muda mrefu ya kifua, HIV n.k.
 Watoto wadogo walio chini ya miaka mitano.
 Wazee walio na umri wa zaidi ya miaka 65 na zaidi.
 Wagonjwa wenye matitizo ya asthma.
 Wagonjwa wanotumia dawa za kudhoofisha mfumo wa kulinda mwili au (immunosuppression).
…. Naam, usikose kujua namna ya kujikinga na kupatwa na ugonjwa huu hatari katika sehemu ya pili

Kila dakika moja mwanamke anafariki dunia akijifungua


Imetangazwa kuwa idadi ya wanawake wanaofariki dunia wakati wa ujauzito na kujifungua imeongezeka katika nchi nyingi. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mfuko wa Idadi ya watu wa Umoja wa Mataifa (UNFPA), kila dakika moja mwanamke mmoj hufariki dunia wakati wa kujifungua.
Katika mkutano uliofanywa na Mawaziri wa Ulinzi kutoka nchi 150 duniani mjini Addis Ababa Ethiopia, kumeripotiwa kuwa uzazi unasababisha idadi kubwa zaidi ya wanawake wapoteze maisha ikilinganishwa na matukio mengineo kama vile vita. Kutokuwepo wakunga wenye ujuzi wa kutosha, na umbali mkubwa kati ya maeno ya vijijini hadi kwenye vituo vya afya ni miongoni mwa sababu zinazochangia matatizo makubwa na vifo vya wanawake wajawazito. Mawaziri hao wamekubalina kwamba, kuzaa kwa mpango ni moja ya njia za kukabilina na matatizo kama hayo na kwamba, inahitajika serikali ziwekeze zaidi katika elimu ya huduma ya afya.

Sunday, November 1, 2009

Idadi ya watu wanaokufa kutokana na homa ya mafua ya nguruwe duniani yaongezeka


Twakimu za hivi karibuni kabisa za Shirika la Afya Dunian WHO zinaonyesha kwamba, zaidi ya watu 700 wanakufa kila wiki kutokana na homa ya mafua ya nguruwe!
Zaidi ya vifo 5,700 viliripotiwa Oktoba 25 ikilinganishwa na vifo 5,000 vilivyotokea wiki moja kabla.
Watu wengi wamefariki zaidi katika maeneo ya Amerika ambapo zaidi ya vifo 4,175 vimeripotiwa. Baadhi ya nchi kama vile Ukraine vimefunga mashule na kupiga marufuku mikusanyiko ya hadhara kama njia ya kukabiliana na mfumuko wa ugonjwa wa homa ya mafua ya nguruwe hasa katika msimu huu wa baridi. WHO imetangaza kwamba, nchi nyingi hazihesabu tena watu wanaopatwa na ugonjwa huo na kwa sababu hiyo basi inakadiriwa kwamba watu walioambukizwa virusi vya H1N1 ni wengi sana duniani.
Ugonjwa wa homa ya mafua ya nguruwe ulianzia nchini Mexico April mwaka huu, na hivi sasa ugonjwa huo umeenea katika nchi nyingi duniani, suala lililopelekea ugonjwa huo kutangazwa kuwa janga la ulimwengu.
Kona ya Afya inawahusia wadau wa globu hii kuzingatia kuosha mikono vizuri kwa sabuni kila mara na kuvaa mask wanapokuwa kwenye mikusanyiko ili kujiepusha kupatwa na homa ya mafua ya nguruwe. Naahidi kuwa hivi karibuni niaelezea kwa kina kuhusiana na ugonjwa huo. Tuzilinde Afya zetu!

Maboga yanaweza kuzuia magonjwa yanayotokana na kuvu au Fungus


Kwa muda mrefu maboga yamekuwa yanajulikana kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kutumika kama dawa, vilevile chakula hicho kina protini yenye nguvu ambayo inaweza kupambana na magonjwa mbalimbali yanayotokana na kuvu au fungus.
Maboga yamekuwa yakitumika sana katika tiba za kiasili katika kutibu magonjwa tofauti kama vile kisukari, shinikizo la damu, kiasi kikubwa cha mafuta mwilini pamoja na saratani katika nchi kama vile China, Korea, India, Yugoslavia, Argentina, Mexico, Barazil na kwingineko.
Kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa kwenye jarida la Kilimo na Kemia ya Vyakula, imeonyeshwa kuwa protini inayotokana na boga iitwayo Pr-2, inapambana vilivyo na ugonjwa unaosababishwa kuvu au fungus wa sehemu za uke (Vaginal yeast infection). Vilevile michubuko inavyotokana na mkojo au nepi (diaper rashes) pamoja na matatizo mengine ya kiafya. Protini hiyo ya Pr-2 iliyoko kwenye maboga halikadhalika inazuia aina 10 za fungus au kuvu ikiwemo aina hatari ya fungus wajulikanao kama Candida Albicans. Fungus hao ni maarufu kwa kusababisha matatizo kwa watu wenye ugonjwa wa kisukari na kupelekea kupata fungus midomoni, katika ngozi, chini ya kucha pamoja na katika mfumo mzima wa mwili.
Waaalamu wana matumaini kuwa, protini hiyo inayopatikana kwenye maboga inaweza kupelekea mafanikio ya kutengezezwa tiba asilia ya kupambana na magonjwa ya kuvu au fungus.
… Haya shime kama ulikuwa unadharau kula maboga, nafikiri inakubidi ufikirie tena!

Saturday, October 31, 2009

Maumivu ya Tumbo la Hedhi... Sehemu ya Pili


kukasababisha mtu kupatwa na maumivu ya tumbo la hedhi. Miongoni mwa magonjwa hayo ni:
• Endometriosis. Hii ni hali ambayo seli za ndani ya mfuko wa uzazi huanza kuoka nje ya fuko hilo, au hta sehemu nyinginezo.
• Adenomyosis: Huu ni ugonjwa wa wanawake ambapo tezi au uvimbe (tumors) zinaoota katika mfuko wa uzazi.
• PID au Ugonjwa wa uvimbe katika nyonga.
• Magonjwa ya zinaa yanayotokana na bakteria au magonjwa ya kuambukiza ya zinaa.
• Mlango wa uzazi unapokuwa mdogo kiasi kwamba unazuia damu ya hedhi isitoke kwa urahisi.
Baada ya kujua baadhi ya matatizo ya wanawake yanayoweza kusabibisha hedhi inayoambatana na maumivu ya tumbo, hebu sasa na tuzijue tumbo la mwezi linaumaje?
1. Maumivu mara nyingi si makali.
2. Muumivu huja na kuondoka, na kwa kiwango tofauti (spasmodic).
3. Maumivu zaidi huhisiwa sehemu ya chini ya tumbo.
4. Huchanganyika na maumivu ya sehemu ya chini ya mgongoni ambayo husambaa mpaka mapajani.
5. Kujihisi kutapika, kichefuchefu na wakati mwingine hata kutokwa jasho.
6. Kupata choo kilaini au hata kuharisha.
7. Kufunga choo.
8. Tumbo kuwa kubwa au kuwa gumu.
9. Kuhisi maumivu ya kichwa.
10. Kutojihisi vizuri au kujisikia kuchoka.
Inapasa kujua kuwa, kiwango cha maumivu ya tumbo la hedhi na mchanganyiko wa dalili inategemea mtu na mtu, mtu mwingine anaweza akawa anapata karibu dalili zote nilizozitaja hapo juu na mwingine ni baadhi tu au hata dalili moja. Wanawake wengi hutambua wanapopata tumbo la hedhi bila hata msaada wa daktari. Wanawake wanashauri iwapo watapata maumivu makali sana ni bora wakamuone daktari ili wafanye vipimo kama vile Ultrasound, CT na CT-Scan, MRI na vinginevyo ili kufahamu iwapo kuma matatizo mengine ya kitiba yanayosababisha maumivu hayo kuwa makali.
Matibabu ya maumivu ya tumbo la hedhi kwa kawaida huweza kutibika kwa urahisi kwa kutumia vidonge vya kupunguza maumivu, kama vile Ibuprofen, naproxen au aina nyinginezo za vidonge visivyokuwa na steroids (NSAIDS). Pia kuna wakati madaktari wanaweza kumshauri mgonjwa kutumia vidonge vya kuzuia mimba, Vidonge hivyo huzuia mzunguko wa yai au Ovulation na kupunguza ukali wa maumivu ya tumbo la hedhi.
Kuna baadhi ya tiba za mitishamba pia ambazo husadia kupunguza muamivu ya tumbo la hedhi. Hapa namaanisha herbal, wenzetu Wachina ni watalamu wazuri katika ujuzi huo. Vilevile wanawake washauriwa kufanya baadhi ya vitendo ambavyo hupunguza maumivu hayo, baadhi ya hivyo vimetaja kama kuoga maji moto, kutumia hot bottle na hata kuweka kitambaa chenye joto katika sehemu ya chini ya tumbo. Kuna baadhi husaidia kwa kufanya mazoezi kama yoga, meditation, kusuliwa, tiba ya sindano (Acupunture), TENS au kushituliwa mishipa ya fahamu ( Transcitaneous Electric Nerve Stimulation na hata wengine husaidiwa kwa tendo la kujamiiana. Vilevile kutumia vidonge vya vitamin E, Thiamine na Omega 3 kumetajwa kuwa husaidia katika suala hilo. Wanawake wanaopatwa na matatizo kama hayo ni bora wapumzike vyema na kupata usingizi wa kutosha.
Tunaelezwa kuwa tunaweza kujiepusha na kupatwa na maumivu ya tumbo la mwezi kwa kufanya yafuatayo:
 Kujitahidi kula matunda, mbogamboga na kupunguza kula vyakula vyenye mafuta mengi, pombe, cofeini, Sodium na sukari.
 Kufanya mazoezi.
 Kujiepusha na wasiwasi na mawazo.
 Kuepuka kufuta sigara.
… Haya kina mama na kina dada, tukumbuke kuwa afya ni zetu na inabidi tuzitunze!