Thursday, November 5, 2009

Namna ya kupima kiwango cha mafuta mwilini kwa kutumia BMI


BMI au Body Mass Index nia njia inayotumiwa kupima uzito wa mwili ukilinganishwa na urefu. Ingawa kipimo hicho hakionyeshi kiwango cha mafuta mwilini moja kwa moja lakini kinaonyesha kiwango cha unene ambao hukadiria hatari ya kupatwa magonjwa mbalimbali. Kipimo cha BMI kinatumika kwa wanawake na wanaume walio na umri wa kuanzia miaka 20 na kuendelea.
Namna ya kuhesabu BMI:
Uzito kwa kiwango cha kilogramu, gawanja kwa meta mraba ya urefu.
Kiwango cha BMI sawa au chini ya 18.5 kinaonyesha kuwa uzito wa mtu ni mdogo chini ya kiwango kinachotakiwa kiafya.
Kiwango cha BMI kikiwa sawa na 18.5 hadi 24.9 kinaonyesha kwamba uzito wa mwili ni wa kawaida na unaotakiwa.
Kiwango cha BMI kinapokuwa kati ya 25.0 na 29.9 kinaonyesha kuwa mtu ana uzito mkubwa.
Lakini kiwango cha BMI kinapokuwa 30 na kuendelea inaonyeshea kuwa uzito wa mtu ni mkubwa mno au ana obesity.
Mbali na BMI vilevile mzunguko wa kiuno au (waist size) unaozidi nchi 40 kwa wanaume na wanawake nchi 35, unaonyesha kuwa mtu yuko katika hatari ya kupata matatizo ya kiafya kama vile kisukari, shinikizo la damu pamoja na magonjwa ya moyo.

No comments: