Saturday, November 28, 2009

Watu milioni 25 wamefariku dunia duniani kote kutokana na UKIMWI


Taarifa ya pamoja ya Shirika la Afya Duniani (WHO) pamoja na shirika la UNAIDS imesema kwamba, idadi ya watu waliofariki dunia duniani kote kutokana na ugonjwa wa Ukimwi imefikia milioni 25. Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyotolewa hivi karibuni, inakadiriwa kwamba watu wengine milioni 33.4 wanaishi na virusi vya HIV duniani. Ripoti hiyo aidha imesema kwamba, karibu watu milioni 60 wakiwemo watu 25 milioni waliofariki dunia, wameambukizwa virusi vya HIV tangu ugonjwa huo ulipoanza. Ingawa idadi ya watu walioambukizwa ugonjwa wa HIV imeongeza, lakini takwimu za watu wanaofariki kutokana na ugonjwa huo, zimepungua ikilinganishwa na huko nyuma.
Matumizi ya dawa za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi au anti-retroviral drugs, yanaaminika kuwa yamepunguza kwa asilimia 10 vifo vinavyotokana na magonjwa yanayoambatana na ugonjwa wa Ukimwi katika miaka mitano iliyopita.
Ripoti hiyo pia imesema kwamba, bara la Afrika bado ni sehemu yenye maambikizo makubwa zaidi ya virusi vya Ukimwi ikilinganishwa na sehemu nyinginezo duniani na kwamba ugonjwa huo unasababisha nusu ya wakinamama wanojifungua kufariki dunia katika bara hilo.

No comments: