Saturday, November 7, 2009

Tibu chunusi kwa kutumia limau!


Limau kulina tindikali aina ya citric ambayo inasaidia kuponya chunusi. Vilevile tunda hilo lina Vitamin C ambayo ni muhimu katika kuifanya ngozi iwe na afya wakati alkali inayopatikana katika limau nayo husaidia kuua vijidudu vinavyosababisha chunusi.
Kunywa juisi ya limau kama chakula cha kwanza asubuhi kunaaminika kusadia kuboresha ngozi.
Jinsi ya kutengeneza nyumbani mchanganyiko wa limau kwa ajili ya kutibu chunusi:
• Kwa kutumia pamba paka maji ya limau katika sehemu yenye chunusi na wacha kwa usiku kucha.
• Safisha kwa maji safi asubuhi inayofuata.
• Ingawa unaweza ukahisi kuwashwa wakati unapopatumia mchanganyiko huo juu ya ngozi mara ya kwanza, lakini baadaye hali hiyo huzoeleka.
Au

1. Changanya maji ya limau ulioyakamu kutoka katika kipnde kimoja cha limao na changanya na maji ya waridi (rose water) au asali nyepesi kwa kiwango hicho hicho.
2. Paka mchanganyiko huo katika sehemu za ngozi zenye chunusi na subiri kwa muda usiopungua nusu saa mpaka saa lizima.
3. Baadye osha kwa maji.
Mchanganyiko huu unapaswa kupakwa mara mbili kwa siku, bora utumiea asubuhi na jioni.
Muhimu: kutumia mchanganyiko huu hakuna madhara na ni wa asilia, lakini iwapo chunusi zinazidi au kuna vidonda vinavyoambatana na chunusi ni bora upate uchauri wa daktari kwanza.

No comments: