Saturday, November 14, 2009

Leo ni Siku ya Kimataifa ya Ugonjwa wa Kisukari



Leo ni Jumamosi tarehe 14 Novemba ambayo ni siku ya kimataifa ya ugonjwa wa kisukari au diabete. Hii ni siku ambayo kampeni za tahadhari hufanywa dunia nzima kuhusiana na ugonjwa wa kisukari. Kwa ajili hiyo Shirika la Afya Dunia (WHO) pamoja na taasisi nyingine za Tiba na Afya duniani, zikishirikiana na madaktari, wataalamu na wadau wa Afya uliwemnguni kote, hutumia siku hii ili kuelimisha na kufunza zaidi jamii kuhusiana na ugonjwa wa kisukari. Taasisi ya Kisukari ya Kimataifa inakadiria kuwa watu milioni 344 duniani wako katika hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari aina ya pili, au Type 2 Diabates. Idadi hiyo ni sawa na idadi yote ya wananchi wa Marekani, iwapo utawahesabu wakaazi wa California mara mbili. Taasisi hiyo pia imetangaza kuwa, watu milioni 285 tayari wanasumbuliwa na ugonjwa huo duniani kote.
Kwa mnasaba huo basi Kona ya Afya inachukua fursa hiyo kuelezea ni nini ugonjwa wa kisukari?
Kisukari ni ugonjwa unaotokea pale mwili unaposhindwa kusaga vyema chakula ili kutoa nishati na kusaidia ukuaji wa mwili. Kila tunachokula husangwa na kubadilishwa kuwa glukosi. Glukosi ni aina ya sukari kwenye damu ambayo ndio chanzo cha nishati au kama mafuta kwa ajili miili yetu.
Baada ya chakula kuyeyushwa hushika njia kuelekea katika damu. Seli zetu za mwili hutumia glukosi kama chanzo cha nishati na kukua. Hata hivyo, glukosi haiwezi kuingia katika seli zetu za mwili bila kutumia wenzo unaoitwa insulini. Insulin huwezesha seli zetu za mwili kuchukua glukosi. Insulini ni homoni ambayo inatengenezwa na kongosho au pancreases.
Tukishwa kula chakula, kongosho zenyewe hutoa kiasi cha kutosha cha insulini kinachoweza kuhamisha glukosi iliyoko kwenye damu kwenda kwenye seli, na kwa njia hiyo kiwango cha sukari katika damu hupungua.
Mtu mwenye kisukari ana hali ambayo kiwango cha sukari katika damu yake kiko juu sana au hyperglycemia. Hii husababishwa na moja kai ya hali tatu zfuatazo. Moja ni kwa sababu mwili huwa hauwezi kutoa kiasi cha Insulini inayotakiwa . Mbili ni pale inapokuwa hakuna insulini inayotengenezwa mwilini, na tatu ni pale seli za mwili zinapokuwa hazishughuliswi ipaswavyo na insulini inayotengenezwa na kongosho.
Matokeo ya hali hizo hupelekea kujikusanya sukari kwa wingi katika damu. Sukari hiyo nyingi kwenye damu polepole hutoka nje ya mwili kama mkojo. Hivyo, ingawa damu ina kiasi kikubwa cha sukari, lakini seli za mwili haziwezi kuitumia sukari hiyo ili kukidhi mahitaji muhimu ya kuupatia mwili nishati na nishati na kwa ajili ya kukua.
Kuna aina tatu za Kisukari.
1. Kisukari aina ya kwanza au Diabates Type 1, aina hii hutokea pale mwili unaposhindwa kuzalisha insulini kabisa.
2. Kisukari aina ya pili au Diabates Type 2, aina hii hutokea pale mwili uanapozalisha insulini lakini insulini hiyo ikawa haiwezi kutumika ipaswavyo.
3. Kisukari cha Ujauzito au Gestational Diabates, kisukari cha aina hii hutokea wakati wa ujauzito.
Inafaa kufahamu kuwa kisukari aina ya kwanza na ya pili ni magonjwa sugu, ikimaanishwa kuwa ni ugonjwa unaoendelea na kwa kawaida mara nyingi hautibiki na kumalizika, bali mgonjwa hubakia nao umri wake wote. Lakini kisukari cha wakati wa ujauzito kwa kawaida hutokea tu wakati huo wa mamba, na baada ya mtoto kuzaliwa ugonjwa huo huisha.

No comments: