Wednesday, November 11, 2009

Vyakula vinavyosaidia mwili kujilinda na maambukizo ya homa ya mafua ya nguruwe



Kula karoti, uyoga, komamanga na chai ya kijani ( green tea) kunasaidia kuulinda mwili katika kukabilina na kupatwa na ugonjwa wa homa ya mafua ya nguruwe.
Kama mnavyojua kila siku zinavyokwenda, ndivyo idadi ya watu wanaopatwa na influenza aina ya H1N1 inavyoongezeka duniani kote, basi tunapaswa kujua namna ya kuilinda miili yate ili kuepuka kupatwa na ugonjwa huo. Wataalamu wameelezea vyakula kama vile karoti, uyoga, komamanga na chai ya kijani huufanywa mfumo wa kulinda mwili kuwa na uwezo wa kukabiliana na virusi hivyo hatari vinavyosababishwa hama ya mafua ya nguruwe.
 Karoti zinaonekana kufaa sana katika suala hilo kwani zina mada ya beta carotine husaidia mwili katika kukabiliana na ugonjwa huo. Imeonekana kuwa kila betacarotine inavyokuwa mwilini kw aingi ndivyo seli za kulind amiwli zinavyoongezeka.Basi tutumie karoti katika vyakula vyetu ikibidi kila siku. Tunaweza kutengeneza saladi, juice ya karoti au hata maji ya karoti na maziwa.
 Uyoga nao vile vile huimairisha kinga ya mwili na ni chakula kinachoupatia mwili protini pia. Tunaweza kupika uyoga kama mboga au kuutumia katika saladi, sosi au kuuchanganya katika vyakula vinginevyo kama vile pizza n.k.
 Komamanga ni tunda ambalo linasifika sana kwa kuwa na uwezo wa anti oxidanti ambapo anti oxidant huzuia radikali huru ambazo ni hatari sana kwa mwili wetu. Uwezo huo humepekea mwili kukabilina na magonjwa mbalimbali ukiwepo ugonjwa wa homa ya mafua ya nguruwe. Kama huwezi kupata tunda la Komamanga sokoni, basi unaweza kutumia juisi ya kamamanga.
 Chai ya kijani (Green Tea) ina aina mojawapo ya anti oxidanti inayojulikana kama Catechin ambayo huweza kuongeza seli za kulinda miwli. Wataalamu wanasema kuwa Catechin huvipavya virusi vya homa ya mafua ya nguruwe visiweze kusambaa mwbilini.Tusisahau pia kuwa mojawapo ya faida za chai ya kijani ni kuwa husadia kuongeza umri wa mtu na kuimarisha mfumo wa kulinda mwili.

No comments: