Friday, November 20, 2009

Seli mama zinaweza kutengeneza ngozi mpya kwa walioungua moto


Wataalamu wa Ufaransa wamesema kuwa, wamegundua njia mpya ya kutumia seli mama za kiini tete cha mwanaadamu (human embryonic stem sells) kutengeneza ngozi mpya ambayo inaweza kutumika kwa watu waliongua na moto. Wamesema kuwa, katika uchunguzi wao seli mama imeweza kuota na kuwa ngozi kamili, wiki 12 baada ya kupandwa katika panya wa maabara. Wataalamu hao wameonyesha matumaini yao kwamba, ngozi hiyo inaweza kutatua tatizo la kuangaliwa vibaya na hata kukataliwa wagonjwa walioungua vibaya na moto katika jamii. Wataalamu wa seli mama wamesema kwamba, ugunduzi huo ni mafanikio muhimu.
Kwa zaidi ya miaka 20 sasa wagonjwa walioungua vibaya kwa moto wamekuwa wakitumia teknolojia inayokuza ngozi mpya katika maabara, lakini kwa kutumia seli za ngozi zao wenyewe. Lakini teknolojia hiyo inachukua wiki tatu, suala ambalo linamfanya mgonjwa aliyeungua akabiliwe na hatari ya kupoteza maji ya mwili na kupata maradhi mbalimbali au infection.

No comments: