Monday, November 30, 2009

Binadamu anaweza kusikia kwa kupitia ngozi!


Huku masikio yakiwa hayachukuliwa tena kuwa ni njia pekee ya kusikia mwanadamu, uchunguzi mpya umeonyesha kuwa ngozi pia inaweza kusaidia katika kuleta kusikia. Chunguzi za huko nyuma zilionyesha kuwa, ishara za macho kama vile mzungumzaji kutikisa kichwa zinaweza kuwa kuathiri namna mtua navyosiakia kitu. Na pia inajulikana kuwa zaidi ya masikio suala zima la kusikia sauti hufanywa pia kwa kupitia mifupa ya kichwa. Uchunguzi mpya hata hivyo umehitimisha kwamba kuna masuala mengineyo zaidi ya ishara za kusikia na macho ambazo zinaathiri suala zima la kusikia. Kwa mujibu wa utafiti huo uliochapishwa katika Jarida la Nature, binadamu wanaweza kutafisiri sio tu ishara zilizotolewa kwa macho, bali pia huweza kutafisri taarifa wanazohisi kupitia ngozi zao wakati wanaposikia jambo. Wanasayansi wana matumaini kwamba ugunduzi wao huo utafungua njia ya kuimarishwa vifaa vya mawasiliano kwa ajili ya watu wasiosikia vyema.

No comments: