Thursday, December 3, 2009

Dalili za mshituko wa moyo… sehemu ya mwisho


Leo tutazungumzia dalili za mshitiko wa moyo na hivyo kukamilisha mada ya mshituko wa moyo.
Baadhi ya wakati mshituko wa moyo hutokea kwa dalili zilizo wazi na kwa haraka sana. Lakini mara nyingi mshituko wa moyo hutekea polepole huku mtu akipata mauvimu ya wastani na kutokujisikia vyema. Mara nyingi watu wanaopatwa na hali kama hiyo huwa hawana uhakika na kile kinachotokea na husubiri kwa muda mrefu kabla ya kuomba msaada au kumuona daktari. Zifuatazo ni dalili ambazo hutekea pale mtu anapopatwa na mshituko wa moyo.
• Maumivu katika kifua: Mara nyingi mtu anapopatwa na mshituko wa moyo huhisi maumivu sehemu za kifua hasa sehemu za katikati ya kifua ambayo huweza kuisha baada ya dakika kadhaa au mara nyingine maumivu hayo huisha na kurudia tena. Mtu huhisi kana kwamba kifua kinabana, kimejaa na kinauma.
• Maumivu katika sehemu za juu za kiwiliwili: Mtu anaweza akajihisi maumivu sehemu za mikono, mgongo, shingo, taya na tumbo.
• Kukosa pumzi au kushindwa kupumua: Hali hii huweza kutokea ikichanganyika na maumivu ya kifua au bila maumivu hayo.
• Dalili nyinginezo: Dalili nyinginezo ni pamoja na kutoka kijacho chembemba (cha baridi), kujisikia kichefuchefu pamoja, kichwa kuwa chepesi na kizunguzungu.
• Moyo kwenda mbio. Kuhisi mapigo ya moyo yanapiga zaidi kuliko kawaida.
Unashauriwa iwapo utajiskia mumivu ya kifua, hasa pamoja na mchanganyiko wa moja wa dalili tilizotaja hapo huu, usisubiri zaidi ya dakika na haraka mpigie simu daktari au wasiliana na kituo cha afya ili upatiwe msaada. Au haraka elekea hospitali mwenyewe. Muda unaofaa wa kutibiwa mshituko wa moyo ni saa moja tangu wakati hali hiyo ilipotokea. Kutibiwa mapema dalili za mshituko wa myo hupunguza hatari ya kuharibika seli za moyo. Hata kama huna uhakika dalili unazohisi ni za mshituko wa moyo, ni bora umuone daktari na ufanyiwe uchunguzi.
Utafiti waliofanyiwa wanawake 515 ambao walipata mshituko wa moyo umeonyesha kuwa, wengi wao waliripotiwa kuwa na dalili za kujihisi kuchoka, kutokulala vyema, kushindwa kupumua, kujisikia maumivu baada ya kula na wasiwasi. Asilimia 70 ya wanawake hao walihisi dalili zisizopungua moja kabla ya kupatwa na mshituko wa moyo.

No comments: