Wednesday, December 16, 2009

Sumu ya Ndani ya Chakula au Food Poisoning…sehemu ya mwisho


Mambo mengi yanaweza kufanywa ili kuzuia vijidudi maradhi na sumu kuchafua chakula chetu. Mosi, safisha mikono yao kwa utaratibu, kabla na kila mara unapotayarishah chakula, funika kwa sashi au bandage sehemu yoyote ya yenye mchubuko au uliojikata katika mkono wako kabla ya kuanza kuandaa chakula,safisha sehemu zote utakazotumia wakati wa maandalizi ya chakula, brashi na sponji za kuoshea vyombo kwa kiasi kikubwa huwa na uwezekano wa kubeba bacteria. Kwa hivyo ni lazima zioeshwe mara kwa mara baada ya kutumia. Vyakula aina ya nyama na mayai vinapaswa kupikwa barabara na vipoti kupashwa moto vizuri kabla yakuliwa. Hakiisha jokofu au friji lako lina nyuzi joto 40 na freeza ikiwa nyuzi 0 au chini ya hapo, kiporo cha chakula kisikae ndani ya jokofu kwa zaidi ya siku nne, usiache ovyo nyama bila ya kuihifadhi, na vyema uichemshe kwa zaidi ya nyuzi joto 140, kuwa mwangalifu wakati wa kuhifadhi vyakula kama vile samaki, nyama mbichi na mayai, hivyo vyote vinaweza kuchafuliwa na bacteria wa maradhi. Usivue samaki kutoka kwenye maji yaliyochafuka, safisha mboga mbichi na matunda kabla ya kula au kupika, unanunuji vyakula vinavyouzwa ndani ya makopo, mikebe n.k unapaswa kwanza kuangalia muda wa matumizi yake unakwisha lini, usile uyoga wa mwituni, ambao haujaidhinishwa na mtaalamu kuwa ni salama kwa mwanadamu na mwisho hakikisha kuwa bidhaa zote zinazotokana na maziwa ambazo nyingi huuzwa madukani ni lazima ziwe zimeondolewa vijidudu hasa bacteria kwa njia ya kitaalamu ijulikanayo kama pasteurization. Maziwa ya ng'ombe ambayo hayajapitia katika njia hiyo ya pasteurization, yanapaswa kuchemshwa vizuri kabla ya kutumia.
Itakumbukwa kuwa watoto, wazee na wale wote wenye magonjwa ya muda mrefu au wenye kinga ya dhaifu ya mwili huwa na hali mbaya wakati wakila chakula kilichoharibika au kuchafuliwa na vimelea vya maradhi. Kwa hiyo ili kukabiliana na tatizo hili, watu wazima wanapaswa kubeba jukumu kuu la kuepukana na suala hilo na vile vile kuwaelekeza watoto pia nini cha kufanya.

No comments: