Sunday, December 6, 2009

Kuvuta sigara mara baada ya kuama kunaongeza hatari ya kensa ya mapafu


Wanaovuta sigara mara tu baada ya kuamka asubuhi, husababishwa kiwango cha juu cha nikotini kukusanyika katika damu zao, zaidi ya wale wanaofuta sigara baadaye, suala ambalo huwafanya wakabiliwe na hatari kubwa zaidi ya kupatwa na kensa ya mapafu. Kuvuta sigara baada ya kupata kifungua kinywa, huunguza kiwango hicho cha nikotini katika damu. Uchunguzi umeonyesha kwamba, wafutaji sigara wa mapema asubuhi, huongeza kiwango kikubwa cha nikotini katika damu zao, bila kuzingatia kwamba wanavuta sigara ngapi kwa siku. Uchunguzi uliofanywa na Chuo Kikuu cha Tiba cha Penn State umeshauri kwamba, wanaovuta sigara mapema asubuhi wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi ya kupata kensa ya mapafu, hivyo ni bora wasaidiwe kuacha kuvuta sigara. Ingawa sababu inayopelekea kiwango cha nikotini kiwe juu zaidi kwa wafuta sigara kabla ya kula stahtahi haijafahamika, lakini inaonekana kuwa wale wanaovuta sigara kabla ya kula kitu wamebobea zaidi katika uvutaji, ikilinganiswa na wale wanaosubiri na kuvuta sigara baadaye.
Inafaa kujua kuwa: Uvutaji sigara unasababisha kwa asilimia 90 vifo vinavyotokana na kensa ya mapafu. Idadi ya watu wanaopatwa na kensa ya mapafu inaongezeka kila siku duniani na kuzidisha vifo vinavyotokana na saratani nyinginezo.
Kwa kawaida kensa ya mapafu huwapata watu wanapokuwa na umri wa miaka 45, na wakati mtu anapopimwa na kukutwa na ugonjwa huo kwa kawaida huwa tayari umeshasambaa mwilini mwake. Saratani ya mapafu inahusiana moja kwa moja na uvutaji sigara. Hatari ya kupatwa na kensa ya mapafu inaambatana moja kwa moja na idadi ya sigara mtu anazovuta.

No comments: