Monday, December 14, 2009

Oooh! Jeli ya HIV ya kina mama imeshindwa kuzuia Ukimwi!


Jaribio kubwa la jeli ya ukeni ya kuzuia vijidudu limeonyesha kuwa, hakuna ushahidi kwamba inapotumiwa huuzuia hatari ya maambukizi ya Ukimwi kwa wanawake. Jeli jiyo inayoitwa PRO 2000, ilikuwa inakusudiwa kutumiwa kabla ya kujamiiana ili kusaidia kupunguza maambukizo ya Ukiewi. Jaribio hilo lilifanywa kwa kuwashirikisha wanawake 9,385 katika nchi 4 za Kiafrika. Ilikuwa inatarajiwa kuwa jeli hiyo ya kuzuia vijidudu ingeweza kuwa njia muhimu ya kupunguza kuenea kwa virusi vya HIV, huku wataalamu wakikiri kwamba kuenezwa kondom pekee hakujasaidia kupunguza maambukizo ya ugonjwa huo. Wataalamu wanasema kuwa bado njia mpya zinahitajika zaidi ili kupambana na gojwa hilo hatari, hasa katika nchi zilizo chini ya jangwa la Sahara barani Afrika, ambapo zaidi ya asilimia 70 ya wale walioambukizwa ugonjwa huo ni wanawake. Wanawake mara nyingi wamekuwa wakilazimika kufanya ngono zembe, na wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi ya kupatwa na ugonjwa wa Ukimwi kuliko wanaume, hivyo inafikiriwa kuwa iwapo itapatikana jeli ambayo wataweza kutumia ili kuzuia maambukizo hayo, suala hilo litawalinda zaidi.
Huko nyuma jaribio dogo lilionyesha kwamba jeli aina ya PRO 2000 ingeweza kupunguza hatari ya mambukizo ya HIV kwa asilimia 30.

No comments: