Monday, December 7, 2009

Watoto wanaozaliwa na uzito mdogo hubaleghe mapema


Kuna ushahidi kuwa watoto wanaozaliwa na uzito mdogo, hufikia baleghe mapema. Jarida la ripoti za lishe za Marekani limearifu kwamba, kuongezeka kwa haraka uzito wa mtoto katika umri wa miaka miwili ya mwanzo, pia kunapeleka kubaleghe mapema mtoto huyo. Kubaleghe mapema pia kumekuwa kukihusishwa na ongezeko la hatari ya kupatwa na kensa za matiti na korodani. Hii si mara ya kwanza utafiti kuonyesha kwamba uzito mdogo wakati wa kuzaliwa unaweza kusababishwa mtoto kukua mapema. Wataalamu wanasema kuwa, kueleweka vyema sababu zinazotokea mapema katika maisha na kupelekea hatari ya kupatwa mtu ugonjwa wa kensa, kunaweza kusaidia katika kuchukuliwa stratejia za kuzuia ugonjwa huo mapema.
Miongoni mwa sababu zinazosababisha mtoto kuzaliwa akiwa na umri mdogo ni:
• Matatizo ya fuko la uzazi
• Rubella
• Mama kuwa na ugonjwa wa Ukimwi
• Mama kutumia pombe kwa wingi wakati wa ujauzito
• Mama kuvuta sigara wakati wa ujauzito
• Mama mjamzito kuwa na magonjwa sugu
• Shinikizo la damu wakati wa ujauzito
• Mama mjamzito kukosa lishe bora
• Mama mjamzito kutumia madawa ya kulevya
• Kuwepo maji mengi kwenye fuko la uzazi.
• Mama mjamzito kuwa na kifafa cha mimba (Preeclampsia)
• Fuko la uzazi kuvunjika kabla ya muda wake
• Mama mjamzito kuwa na magonjwa ya mfumo wa mkojo (U.T.I)
• Matatizo ya urithi
• Mama mjamzito kuwa na matatizo ya figo

No comments: