Sunday, December 13, 2009

Afya njema inaongeza uwezo wa akili au IQ


Utafiti mpya umeonyesha kwamba kuna uhusiano kati ya afya njema ya mwili wa vijana na watu wazima pamoja na kufanya kazi vyema ubongo, na uwezo wa kupata maksi za juu katika vipimo vya akili au IQ test. Utafiti huo uliochapishwa katika jarida la Akademia la sayansi umeeleza kwamba, kuwa na afya nzuri ya mwili katika umri wa miaka 15 na 16 kunaongeza uwezekano wa kuwa na uwezo wa akili wa juu. Wataalamu wamesema vijana wa aina hiyo wana uwezo mkubwa wa kufanikiwa kusoma elimu ya juu na kupata kazi nzuri maishani. Kuwa fiti kimwili inaamisha pia kuwa na moyo unaofanya kazi vizuri na uwezo mkubwa wa mapafu, vilevile kuwa na ubongo wenye kupokea vyema hewa ya oxygen, suala ambalo wataalamu wanasema linatofautiana na kuwa na nguvu za misuli. Wanasayansi wanaamini kuwa, sababu za kimazingira zinaathiri zaidi afya ya mtu na kiwango cha akili kuliko sababu za kurithi.

No comments: