Sunday, December 6, 2009

Kutumia simu ya mkono, hakuna uhusiano wowote na saratani ya ubongo


Japokuwa kumekuwa na imani kwamba kutumia simu ya mkono kwa muda mrefu kunaongeza hatari ya kupatwa na kensa ya ubongo, lakini utafiti mpya umekanusha madai hayo. Huko nyuma uchunguzi ulionyesha kwamba kukaririwa sumaku umeme za redio zinazotoka katika simu za mkono, kunasababisha hatari kubwa ya kupatwa na kensa. Lakini kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa katika Jarida la Taasisi ya Kensa, hakujakuwa na mabadiliko yoyote kuhusiana na ugonjwa wa kensa ya ubongo tangu simu za mkono zilizpogunduliwa katika muongo wa 1990.
Wataalamu wanasema kwamba, kuna ushahidi wa kisayansi unaosema kuwa, kutumia simu za mkono kwa miaka isiyozidi 10 hakuongezi uwezekano wa kupatwa na saratani, na utafiti huo unaunga mkono suala hilo. Hata hivyo wataalamu wameshauri kuwa, uchunguzi na ufuatiliaji wa muda mrefu unatakiwa kufanywa, kwani uvimbe wa ubongo kwa kawaida unachukua muda mrefu sana hadi unapotokea.
Si vibaya kujua kuwa, utafiti huo umetolewa baada ya kuchunguzwa kesi 59,684 za kensa ya ubongo zilizookea katika miaka 30 tangu mwaka 1974 hadi 2003 kati ya watu wazima milioni 16.

No comments: