Monday, December 14, 2009

Haya tena…. kukoroma kuna uhusiano na kisukari!


Uchunguzi mpya umeonyesha kwamba, wale wanaokoroma wakati wakilala, wanakabiliwa na hatari kubwa ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari kuliko wale wanaolala kimya. Kwa mujibu wa uchunguzi huo uliofanywa kwenye chuo kikuu cha Yale, wale wanaokoroma sana wanapolala, wanakabiliwa na uwezekano wa kupata kisukari kwa asilimia 50. Wataalamu wanasema pia kuwa, kushindwa kupumua usingizini au kitaalamu kunahusiana na kisukari aina ya pili, bila kujali sababu nyinginezo kama vile umri, jinsia, uzito na hata asili anayotoka mtu.
Kukoroma sugu, au kitaalamu sleep apnea ni hali ambayo inasababishwa kushindwa kufanya kazi njia ya hewa, suala ambalo humfanya mtu aamke mara kadhaa usingizini wakati anapolala. Hali hiyo inahusiana na baadhi ya mabadiliko ya umetaboli au hali ya ujenzi wa seli na uvunjaji vunjaji wa kamikali mwilini, kwa kimombo ‘metabolism’.

No comments: