Wednesday, December 30, 2009

WHO yasema, ni mapema mno kutangaza ushindi dhidi ya virusi vya H1N1


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani WHO amesema kuwa ni mapema mno kuweza kutangaza ushindi dhidi ya virusi vya homa ya mafua ya nguruwe akiashiria uwezekano wa virusi hivyo kubadili sura yake na kuwa hatari kubwa zaidi kwa mwanadamu. Margaret Chan amesema kuwa virusi vya H1N1 bado vinaendelea kuzagaa na tayari vimewasibu mamilioni ya watu. Mkuu wa Shirika la Afya Duniani amesema habari njema ya kitiba kuhusu virusi hivyo ni kupungua kasi yake licha ya kwamba vimekwisha sababisha vifo vya watu 12 elfu wengi wao wakiwa wanawake waja wazito, watoto wadogo na watu wenye maradhi sugu. Chan amesema idadi hiyo rasmi ya watu waliofariki dunia kutokana na virusi vya mafua ya nguruwe haiakisi ukweli wa mambo na kwamba idadi kamili ya wahanga wa ugonjwa huo itajulikana baada ya kupita miaka miwili.

No comments: