Saturday, January 2, 2010

Ujue ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB)….sehemu ya pili


Wadau wapenzi mnaofuatilia makala mbalimbali katika blogi ya Kona ya Afya, natumaini mlifaidika na sheemu ya kwanza iliyozungumzia ugonjwa wa Kifua Kikuu. Hii ni sehemu ya pili ambapo leo tunaangalia vipimo vinavyotumika kujua iwapo mtu ameambukiza kifua kifuu. Vipimo vinavyotumia sasa katika nchi nyingi hususan katika ulimwengu wa tatu ni ni kipimo cha picha ya kifua au x-ray, kipimo cha makohozi, kipimo cha ngozi au Mantoux test. Iwapo vipimo hivyo vitathibitisha kuwa mtu amemabukizwa kifua kikuu, mtu huyo atapaswa kutibiwa kikamilifu kwa kufuata ushauri wa daktari ili kuutokomeza ugonjwa huo. Wadau wapenzi baada ya kufahamu nini maana ya Tb, chanzo chake na dalili zake, sasa ni vyema tuelewe matibabu yake. Je, Kifua Kikuu kinaweza kutibika? Jibu ni ndiyo. Kuna dawa aina ya antibiotic ambazo ni tiba barabara ya kuitokomeza Tb lakini chini ya ushauri wa daktari. Itakumbukwa kuwa Shirika la Afya Duniani WHO limetoa mwongozo mpya wa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu kwa kutumia dawa za mseto (fixed dose combination drugs au FDCs) ambazo hutumika sasa katika nchi nyingi za ulimwengu ili kupunguza muda wa matibabu kutoka miezi minane hadi sita. Jambo muhimu la kuzingatia katika utumiaji wa dawa hizo ni kuwa, ni vyema mgonja atumie dawa hizo kama alivyoshauriwa na mtaalamu wa afya na kumaliza dose yake aliyoandikiwa. Kwa hiyo kuna haja ya mgonjwa kuwa chini ya uangalizi maalumu ili kuruhusu ufanyaji kazi wa antibiotic na kuleta athari nzuri kwa mgonjwa. Pili kuna chanjo ya BCG. Hii ni chanjo ambayo hutolewa kwa mtoto mara baada ya kuzaliwa. Chanjo hii humlinda mtoto na kifua kikuu. Hata hivyo katika nchi nyingine chanjo hii hutolewa baadaye kwa watoto ambao wako katika hatari ya kuambukizwa ugonjwa wa kifua kikuu.
Hebu sasa na tunagalie ni chakula gani anachopaswa kula mgonjwa wa TB. Mgonjwa aliye na kifua kifuu anatakiwa kula mlokamili wenye mada za proteini, vitamini na cabohyadarate. Vyakula vya protini ni pamoja na mayai,maziwa,maharage na soya. Vyakula hivyo hujenga misuli na kuzalisha chembe za uhai. Vilevile husaidia mfumo wa kinga ya mwili kupata nguvu. Vile vile ni vyema mgonjwa wa TB apate vitamini zitokanazo na mafuta na mboga za majani. Vyakula hivyo huongeza nguvu na kukinga mwili wake khususan ngozi. Chakula aina ya carbohydrate ambayo inapatikana katika chakula cha nafaka mfano wa mahindi na ngano na vilevile sukari itokanayo na matunda navyo vina umuhimu mkubwa.
Hii ni kwa sababu vyakula hivyo huleta nguvu katika mwili wa mwanadamu. Vile vile bila kusahau maji safi na salama yanayohitajika mwilini. Makala hii itaendelea na msikose kuungana nami tena ili kujua namna ya kujikinga na kifua kikuu. Tutunze Afya zetu daima!

No comments: