Saturday, January 2, 2010

Wanasayansi watengeneza mashine ambayo ni sawa na tumbo la mwanadamu


Wanasayansi wametengeneza mashine ambayo inafanya kazi kama tumbo la mwanadamu. Mashine hiyo imetengenezwa na watafiti wa Kitengo cha Uchunguzi wa Chakula cha Norwich. Mashine hiyo ina uwezo wa kufanya kila aina ya kazi zinazofanyika tumboni, na ina hali mbalimali za kibiokemikali zinazopatikana katika tumbo. Wanasayansi wametengeneza mashine hiyo ili iwasaidie katika uchunguzi wao kuhusiana na chakula katika tumbo la mwanadamu. Mashine hiyo imechukua miaka 10 kutengenezwa na itatumika katika majaribio ya dawa katika mfumo wa chakula. Waliotengeneza mashine hiyo wana matumaini kuwa, mashine hiyo itakuwa msaada mkubwa katika majaribio ya dawa ambayo ni vigumu kujaribishwa kwa mwanadamu kwenye viwanda vya kutengenezea madawa. Martin Stock msemaji wa Kiwanda cha Boioscience Ltd kilichotengeneza mashine tumbo hiyo amesema kuwa, kila mtu anafikiria kuwa tumbo ni kama mfuko ulijaa tu maji na vimeng'enya (enzymes), lakini si hivyo bali tumbo ni sehemu yenye viungo vingi tofauti tofauti, na mashine hiyo inashabihiana kikamilifu na tumbo la mwandamu.

No comments: