Wednesday, January 20, 2010

Jinsia ya mtoto kupimwa kwa kupitian damu


Uchunguzi mpya umeonyesha kwamba, wazazi wataweza katika siku zijazo kujua jinsia ya watoto wao ambao bado hawajazaliwa wakati wa ujauzito kwa kupimwa damu. Kwa kawaida kipimo cha Utrasound huweza kuonyesha jinsia ya kijusi ( fetus) wakati wa miezi mitatu ya pili ya ujauzito. Hivyo, pale inapotakiwa kujua jinsia ya mtoto atakayezaliwa katika wakati wa mwanzo wa ujauzito kutokana na sababu za kitiba, huwa inabidi zitumike njia nyinginezo ambazo ni ngumu zaidi kama vile kupimwa homoni na mada ziliozoko katika maji yanayomzunguka mtoto tumboni au amniocentesis, njia mbayo baadhi ya wakati huweza kuifanya mimba itoke.
Lakini kumepatikana matumaini mapya ya kujua kwa urahisi na mapema jinsia ya mtoto aliyeko tumboni, baada ya uchunguzi uliochapishwa katika jarida la Magonjwa ya Wanawake na Uzazi kueleza kuwa, kipimo hicho cha damu ya mama mjamzito, kinachoweza kufanywa mapema katika wiki ya 7 ya ujauzito, kinaweza kuonyesha kwa uhakika jinsia ya mtoto kijusi. Katika majaribio mbalimbali kipimo hicho kimeonyesha kuwa sahihi kwa asilimia 100, kwa kutumia jeni mbili zinazopatikana katika kromozomu ya jinsia ya Y.
Wataalamu wanaamini kwamna kipimo hicho kitaanza kutumika hivi karibuni na kuchukua nafasi ya njia nyinginezo ngumu na zenye hatari, ili kujua jinsia ya mtoto aliyeko tumboni mapema wakati wa ujauzito, na kusaidia kuamua iwapo mimba itolewe au istolewa pale inapogunduliwa kuwepo kwa baadhi ya magonjwa ya kurithi yanayoambatana na jinsia.

No comments: