Monday, January 4, 2010

Marekani yaondoa rasmi sheria ya kuwazuia waathirika wa Ukimwi kuingia Marekani


Marekani imeondoa marufuku iliyodumu kwa muda wa miaka 22 ya kuwazuia wahamiaji walioathirika na virusi vya HIV/Aids kuingia nchini humo. Rais Barack Obama wa Marekani amesema kwamba sheria hiyo iliyoondolewa, haikuwa inaendana na mikakati ya Marekani ya kuongoza jitihadaza za kupambana na ugonjwa wa Ukimwi. Sheria hiyo mpya ambayo imeanza kutumiwa leo Jumatatu nchini Marekani, huku Washinton ikipanga kuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa Ukimwi kwa mara ya kwanza ifikapo mwaka 2012. Itakumbukwa kwamba marufuku ya kuwazuia waathirika wa Ukimwi wasiingie Marekani iliwekwa mwishoni mwa mwaka 1980, baada ya ugonjwa huo kuanza kutambulika duniani. Marekani ilikuwa ni miongoni mwa nchi 12 ikiwepo Libya na Saudi Arabia ambazo zinazowazuia wageni walioambukizwa virusi vya Ukimwi kuingia katika nchi hizo.

No comments: