Monday, January 25, 2010

FDA yathibitisha na kuitangaza dawa ya kwanza ya kutibu ugonjwa wa MS


Shirika la Kusimamia Chakula na Madawa la Marekani la FDA limethibitisha na kuipitisha dawa ya kwanza iliyotengenezwa kwa ajili ya kutibu tatizo la kutembea kwa wagonjwa wa MS (Multiple Sclerosis). Multiple Sclerosis ni ugonjwa wenye kuudhoofisha mwili kwa kiasi kikumbwa ambapo mfumo wa kulinda mwili hushambulia mfuko unaohifadhi mfumo wa kati wa neva au central nervous system, na kusababisha mwili kufa ganzi na kupooza. Wagonjwa wa MS huwa wanapoteza uwezo wa kutembea na hata kuhitajia msaada wa kibaiskeli ili waweze kutembea. Kwa bahati mbaya hakuna tiba ya ugonjwa huo, ambao unawapata karibu watu milioni 2.5 duniani kote hasa watu wazima. Kwa mujibu wa FDA, wagonjwa wa MS waliopewa dawa hiyo inayojulikana kama Ampyra yenye jina la kitaalamu la Dalfampridine, wameweza kutembea vizuri. Wagonjwa hao wameweza kutembea masafa marefu, kusimama kwa muda mrefu na hata kupanda ngazi kwa urahisi. Watengenezaji wa dawa hiyo wana matumaini kuwa dawa hiyo itaanza kuingia madukani hivi karibuni.

No comments: