Monday, January 25, 2010

Kula Blueberry kunaongeza uwezo wa ubongo


Utafiti mpya umegundua kuwa, kunywa vikombe viwili na nusu vya juisi ya blueberry kwa siku ( mie naziita kunazi za bluu) kunaongeza uwezo wa ubongo wa kufahamu, na kuondoa matatizo ya usahaulifu yanayotokana na utu uzima. Wataalamu wanasema kuwa kunywa kila siku juisi hiyo kunamzuia mtu uwezekano wa kupatwa na ugonjwa wa kupoteza akili uzeeni au wendawazimu. Blueberry kwa kuwa na kiwango kikubwa cha phytochemical, tunda hilo lina limejaa anti oksidanti na lina uwezo wa kuzuia uvimbe. Vilevile kunazi za bluu kwa kuwa na mada iitwayo Anthocyanin, huweza kusaidia kuongeza kumbukumbu katika ubongo. Pia tunda hilo husaidia kupunguza kasi ya kitendo cha kupungua kumbukumbu katika ubongo kwa kuondoa gulukosi zinazopatikana kwenye ubongo. Uchunguzi huo umebaini kwamba, kula blueberry kupitia vidonge maalum vya kusaidia afya au supplements kunaweza kumpatia mtu faida kubwa katika ubongo. Hata hivyo wataalamu hao wameshauri kuwa ni bora tunda hilo liliwe katika hali ya kawaida.
Huko nyuma pia wataaamu walieleza kuwa, Blueberry husaidia kupunguza usongo wa mawazo pamoja na kiwango cha juu cha gulukosi katika damu.
Haya tena wadau…usichelewa kula tunda hili, najua katika nchi zetu za Afrika tunda hili halipatikana na ndio sababu hata jina lake katika kamusi yetu haliko, lakini usife moyo unaweza kupata tunda hilo madukani na katika supermarkets ambapo huhifadhiwa katika makopo au kama juisi. Kwa wale walioko ughaibuni basi hakuna tabu hiyo na usikose kula tunda hilo tamu wakati wa msimu wake na wakati miwngine wowote.
Daima tuzilinde afya zetu!

No comments: