Sunday, January 10, 2010

Chai yaweza kuwazuia wanawake wasipate kensa ya kizazi


Kama wewe ni mwanamke na hupendi kunywa chai itabidi ifikirie tena suala hilo, kwani wanasayansi wamegundua katika uchunguzi wao wa hivi karibuni kwamba, miongoni mwa faida za chai ni kuzuia hatari ya kupatwa na kensa ya kizazi. Huko nyuma pia tafiti mbalimbali zilionyesha faida kemkem za chai. Uchunguzi huo mpya umeonyesha kuwa, chai ambayo ni kinywaji cha pili kunywewa na watu wengi zaidi duniani, inaweza kuzuia kensa ya kizazi (endometrial cancer). Wataalamu wanasema mada ya polyphenols inayopatikana kwa wingi kwenye chai, kwa muda mrefu imeonekana kwamba moja ya faida zake ni kusaidia kupunguza ukubwa wa tezi za saratani, na sasa imegundulika kuwa pia ina faida kwa kensa ya kizazi. Uchunguzi huo umechapishwa katika jarida la Uzazi na Magonjwa ya Wanawake la Marekani, na kueleza kwamba, chai ambayo ina anti oxidanti nyingi inaweza kupunguza uwezekano wa kupatwa na kensa ya kizazi, saratani ambayo ni ya nne kuwapata kwa wingi wanawake nchini Marekani. Hata hivyo wataalamu wamesema kuwa, utafiti zaidi unapaswa kufanywa ili kuthibitisha zaidi utafiti wao huo.

No comments: