Monday, January 11, 2010

Matatizo ya Homoni huwafanya wakinamama wasipende kunyonyesha


Wakinamama wasiopenda kuwanyesha watoto wao wamekuwa wakitupiwa lawama nyingi katika jamii, lakini uchunguzi mpya umeonyesha kwamba huenda hali hiyo ikawa inasababishwa na matatizo la homini mwilini. Kwa mujibu wa uchunguzi uliochapishwa katika Jarida la Uzazi na Magonjwa ya Wanawake la Scandinavia, kiwango cha juu cha homini za testosterone za kiume wakati wa ujauzito, hupelekea wakinamama wasijisikie kunyonyesha baada ya kujifungua. Homoni za testosterone zina athari hasi katika ustawi wa tishu za matezi ya matiti ya kinamama, suala mbalo huathiri uwezo wa mama wa kumnyonyesha mwanaye.
Chunguzi nyingi zimeeleza kumnyonyesha mtoto kuna faida tele kwa afya ya mama na mtoto, huku watoto wanaonyonyeshwa na maziwa ya mama wakionekana kuwa na afya zaidi na kutopatwa na hatari ya kuwa na unene wa kupindukia, wakilinganishwa na wale wanaopewa maziwa ya kopo. Kunyonyesha pia humzuia mtoto asipatwe na magonjwa ya moyo, kisukari, magonjwa kadhaa ya kifua, masikio, shinikizo la damu, ugonjwa wa ngozi (eczema), upungufu wa damu na asthma, huku kukimzuia mama kupata kensa ya matiti.
Uchunguzi huo lakini umesema kuwa, kwa ujumla afya ya watoto wanaopewa maziwa ya kopo haina tofauti sana na ya watoto wanaonyonyeshwa maziwa ya mama. Hivyo wakinamama wasioweza kunyonyesha kutokana na sababu mbalimbali wasijisikie vibaya kutokana na suala hilo, na bora tu kuhakikisha kuwa afya ya mtoto inalindwa vyema.

No comments: