Monday, January 18, 2010

Liche ya Mediterani huzuia hatari ya kupatwa na kensa ya tumbo


Uchunguzi mpya umebaini kuwa, lishe ya Mediterani inaweza kusadia kupunguza uwezekano wa kupatwa na kensa ya tumbo. Lishe hiyo pia ina faida mbalimali kwa afya. Lishe ya Mediterani pia inapunguza hatari ya kupatwa na magonjwa kadhaa kama vile kisukari, magonjwa ya kuzaliwa, magonjwa ya mishipa ya damu, Alzheimer, msongamano wa mawazo na fikra,(depression) uvimbe na vifo vya watoto wachanga. Lishe ya Mediterani ni lishe yenye matunda, mboga mboga, ufumwele samaki, nafaka, mafuta ya zaituni huku nyama nyekundu na vyakula vinavyotokana na maziwa vikiwa kwa uchache.
Inaaminiwa kwamba, lishe nya namna hiyo inamlinda mtu asipatwe na kensa ya tumbo, huku ikisisitizwa kwamba lishe za aina nyinginezo huongeza hatari ya ugonjwa huo. Saratani ya utumbo ni saratani ya pili inayowapata watu kwa wingi ulimwenguni, na wataalamu wanasema kuwa kula lishe ya Mediterani hupunguza uwezekano wa kupatwa na kensa hiyo kwa asilimia 33.
Wataalamu wanawahusia watu kula vyakula ambavyo ni bora kwa afya zao na kuvijua vyakula ambavyo vinawalinda watu wasipatwe na magonjwa mbalimbali kama huo wa saratani ya tumbo.

No comments: