Friday, January 22, 2010

Je, Madawa ya Kudhibiti Virusi vya Ukimwi Yanasaidia Vipi Kuzuia Ukimwi?


Leo nitazungumzia kuhusu dawa za kurefusha maisha ya waathirika wa ukimwi yaani ARV.
Madawa haya huitwa Antiretroviral therapy (ARVs) kwa lugha ya Kiingereza. Dawa hizi hupigana dhidi ya virusi vinavyosababisha ukimwi. Madawa haya huwasaidia wale walio na virusi hivi kukaa katika afya nzuri. Aina nyingine ya madawa haya ni Protease Inhibitors. Aina hii huzingira virusi na kuzizuia kuzaana. Aina mbili hizi za madawa zikitumiwa pamoja, hupunguza idadi ya virusi hivyo na mwishowe hupunguza idadi ya vifo. Takwimu zinaonyesha kuwa watu wengi waliotumia mchanganyiko huo wamepata nafuu. Mfano watu wengine walikuwa wameshindwa kufanya kazi, lakini wameweza kurudi makazini baada ya kutumia madawa hayo.
Matibabu kwa Kutumia Aina Moja ya Dawa (Monotherapy)
Matibabu mengine ya haya ya kutumia dawa aina moja tu. Matumizi haya hupunguza hatari ya kuambukiza virusi hivyo. Kwa mfano kutoka kwa mama hadi kwa mtoto wake mchanga. Tiba ya aina hii haitumiwi sana kwa sababu, mwili hujenga kinga dhidi ya aina moja ya dawa baada ya muda fulani.
Matibabu kwa Kutumia Mchanganyiko wa Madawa (Combination Therapy)
Matumizi ya aina mbili au zaidi wa dawa hizo hutumika kuwasaidia watu wenye ukimwi. Hii ni kwa sababu aina mbali mbali za madawa hupigana na virusi kwa njia tofauti, na kwa hivyo huwa na mafanikio zaidi zinapotumiwa kwa pamoja. Kuna mchanganyiko wa aina tofauti, lakini madawa mengine hayawezi kutumiwa kwa pamoja kwani, yanafanya kazi kinyume cha madawa mengine. Madawa ya aina hiyo yanaweza kutumiwa na watoto kwa kiasi fulani. Lakini ni vyema tukumbushe hapa kuwa watu wengi wanaendelea kuambukizwa virusi ivya ukimwi barani Afrika hasa katika eneo la kusini mwa jangwa la Sahara. Na Imeelezwa kuwa nusu ya maambukizo hayo huwakumba watu wasio na uwezo wa kununua madawa hayo pamoja na kushindwa kuyatumia inavyopasa.
Je utumiaji wa dawa hizo unaweza kuwa njia ya kuzuia ukimwi?
Matumizi ya madawa haya yanaweza kuwa njiai ya kuzuia kuenea kwa ukimwi kwa njia mbili. Mosi kwa kuwatibu watu walioingia kwenye hatari ya kupata ukimwi au kuwapa nafuu watu walio na virusi ili kuzuia maambukizo zaidi kwa wapenzi wao.
Matibabu ya Kuzuia Uambukizo Mara Mtu Anapoingia Katika Hatari (Yaani Post-Exposure Prophylaxis) PEP
Uchunguzi uliofanywa hivi karibuni unaonyesha kuwa, utumiaji wa dawa za AZT mara tu baada ya kudungwa sindano iliyo na damu yenye virusi vya ukimwi, umepunguza maambukizo kwa asilimia 79. Ni vyema kuashiria hapa kuwa, hatari ya wauguzi au matabibu kupata ukimwi baada ya kudungwa na sindano iliyo na damu yenye virusi hivyo ni karibu asilimia 0.32. Hatari ya kupata ugonjwa kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya kwa sindano au kwa kufanya mapenzi, ni kubwa mno pia. Inakadiriwa kwa wale wote wanaofanya mapenzi kwa kutumia sehemu ya haja kubwa wana hatari ya kuambukizwa virusi vya ukimwi kutoka kwa mpenzi aliye na vyo kwa asilimia 0.5 hadi 3 na wale wanaotumia njia ya kawaida kwa asilimia 0.1. Aidha hatari ya kupata ugonjwa wa ukimwi kwa kutumia pamoja sindano ya madawa ya kulevya ni asilimia 0.4 hadi 3.
Nukta ya Kuzingatia:
Matumizi ya madawa haya ya kuongeza muda wa kuishi kwa waathirika wa ukimwi yanahitaji mgonjwa kula chakula bora kila mara, chakula ambacho kinaambatana na madawa haya. Mgonjwa pia anapaswa kunywa maji mengi na kuhakikisha kwamba anahifadhi dawa hizi katika mazingira mazuri. Kwa hiyo dawa hizi hutumiwa na wale walioambukizwa virusi vya HIV baada ya kupima na kushauriwa kiutaalamu hospitalilini au kwenye kituo cha afya na huanza kutumia madawa hayo kulingana na namna alivyoathirika. Mgonjwa anaweza k kutumia madawa haya kwa uarahisi, lakini bado kuna gumu kwa wagonjwa wengi wanaoishi katika hali duni ya maisha. Hofu ya kudhulumiwa, kushukiwa na kubaguliwa yote hayo huwafanywa wagonjwa wengi barani Afrika wakatae dawa hizo za ARV,s.

No comments: