Thursday, December 10, 2009

Watu milioni 5 hufariki dunia kila mwaka kutokana na tumbaku



Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kwamba kila mwaka watu milioni 5 hufariki dunia kutokana na kutumia tumbaku, na kusisitiza kuwa hatua muhimu zinapaswa kuchukuliwa ili kukabiliana na uvutaji wa sigara. Tumbaku inaongoza duniani katika kusababisha magonjwa mbayo yanawezekana kuzuilika. Kuwa karibu na mazingira ya wanaovuta sigara au uvutaji sigara usio wa moja kwa moja (second hand smoking) pia kunasababisha vifo vya watoto 600,000 wanaozaliwa bila kufikia muda wao kila mwaka, huku karibu asilimia 95 ya watu duniani wanaishi katika sehemu ambazo hazina sheria zozote zakupiga marufuku ufutaji sigara. Mkurugenzi wa WHO anayeshughulikia marufuku ya tumbaku Douglas Bettcher amesema kwamba, watu wanapaswa kuelemishwa zaidi juu ya madhara ya tumbaku ambayo ni mabaya kwa afya ya binadamu. Maafisa wa afya wanatabiri kwamba, ifikao mwaka 2030, tumbaku inaweza kusabbaisha vifo vya watu milioni 8 kwa mwaka, hasa katika nchi zilizoendelea, iwapo hatua muhimu hazitochukuliwa ili kupambana na suala hilo.
….Wapenzi wadau wa blogi ya Kona ya Afya, leo wakati nikiandika habari hii nimekuwa nikifikiria ni kwa nini binadamu baadhi ya wakati tushindwe kujizuia kufanya masuala ambayo tunajua fika kuwa ni hatari kwa afya zetu?. Pengine tumesikia mara nyingi kuwa uvutaji sigara una madhara makubwa na tumeshashuhudia hata watu wa karibu yetu wakipata madhara hayo. Labda pia kwa kuwa uvutaji sigara ni suala la kawaida katika nyumba zetu, ofisi zetu, majumba ya starehe, katika mitaa yetu na kote kulikotuzunguka basi tumelizoea suala hilo na kuliona ni la kawaida. Lakini ukweli usiopingika ni kwamba, ufutaji sigara una madhara, sio tu kwa wavutaji sigara peke yao, bali hata kwa sisi tulio karibu ya wavutaji hao. Nafikiri muda umewadia sasa wa kujiuliza kwa undani swali hili kuwa: Je? kama kuna magonjwa yenye madhara kwa afya na uzima wa miili yetu ambayo yanaweza kuepukika, basi kwa nini tusijiepushe nayo!??
Daima tuzitunze afya zetu!

No comments: