Saturday, November 21, 2009

UNICEF yasema, Afghanistan ndiyo sehemu mbaya zaidi ya kuzaliwa mtoto duniani


Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) limesema kuwa nchi ya Afghanistan iliyoharibiwa kwa vita ni sehemu mbaya zaidi duniani ya kuzaliwa mtoto. Shirika hilo limetangaza kwamba, Afghanistan ina idadi kubwa zaidi ya vifo vya watoto duniani ambapo vifo 257 vya watoto hutokea kati ya kila watoto 1,000 wanaozaliwa.
Daniel Toole Mkurugenzi wa Unicef wa kusini mwa Asia amesema kwamba, ripoti yake ya mwaka kuhusiana na watoto duniani imegundua kwamba, Afghanistan ni sehemu hatari kwa wasichana na kwamba kukosekana usalama kumepunguza idadi ya watoto wanaohudhuria shuleni hasa wa kike. Aidha mkurugenzi huyo wa Unicef amelaumu mashambulio ya mara kwa mara ya shule za wasichana ambayo yamesababisha elimu ya wanawake kuporomoka kabisa nchini Afghanistan.

No comments: