Monday, November 23, 2009

Sababu kuu zinazomfanya mtu aweze kupata mshituko wa moyo!..sehemu ya 2


Kwanza tutazungumzi baadhi ya sababu zisizoweza kuzilika zinazosababisha mshituko wa moyo. Nazo ni kama ifuatavyo:-
Kuongezeka umri: Asilimi 83 ya watu wanaokufa na magonjwa ya moyo ni wale waliofikia umri wa miaka 65 na kuendelea. Umri unapokuwa mkubwa, wanawake ambao kwa kawaida hawapatwi sana na ugonjwa moyo, nao pia huanza kukabiliwa na hatari ya magonjwa hayo ukiwemo mshituko wa moyo.
Jinsia ya kiume: Wanaume wanakabiliwa na hatari zaidi ya kupatwa mashituko wa moyo kuliko wanawake, ambapo hupata ugonjwa huo katika umri mdogo. Wanawake baada ya kukatika hedhi au menopause, nao pia huanza kukabiliwa na hatari hiyo lakini si kwa kiasi kikubwa kama wanaume.
Urithi: Watoto ambao wazazi wao wana na magonjwa ya moyo au walipatwa na mshituko wa moyo nao pia wanakabiliwa na hatari ya kupaatwa na magonjwa hayo. Waamerika Weusi wanapatwa na shinikizo la damu zaidi wakilinganishwa na watu wenye asili ya Caucasian au wazungu. Magonjwa ya moyo pia hutokea sana kwa watu wenye asili ya Mexico, India, Hawaii na Asia. Watu ambao familia zao zina historia ya magonjwa ya moyo wanakabiliwa na hatari ya kupatwa na mshituko wa moyo mara mbili zaidi kuliko wengine, kwani mtu hawezi kuchagua umri wake, jinsia na asili yake.
Zifuatazo sasa ni baadhi ya sababu zinazoweza kuepukika zinazosababishwa mshituko wa moyo:-
 Kuvuta sigara: wavuta sigara wanakabiliwa na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo mara 2 hadi 4 zaidi ya watu wasiovuta sigara. Uvutaji sigara ni sababu kubwa inayojitegemea inayoweza kusababisha mshituko wa moyo kwa wagonjwa wenye maradhi ya moyo. Kuvuta sigara hadhani au mbele ya wengine kunawafanya watu hao nao wakabiliwe na hatari hiyo magonjwa ya moyo.
 Kiwango kikubwa cha mafuta katika damu au High Blood Cholesterol: Kila kiwango cha mafuta kinapoongezeka katika damu ndio uwezekano wa kupatwa na magonjwa ya moyo nao unavyoongezeka. Iwapo mtu atakuwa na sababu nyinginezo kama ufutaji sigra, shinikizo la damu na kadhalika, basi mtu huyo ana uwezekano mkubwa zaidi wa kupata shinikizo la moyo. Kiwango cha mafuta katika damu pia kinathiriwa na umri, jinsi, urithi na lishe.
 Shinikizo la damu: Shinikizo la damu huongeza ufanyajikazi wa moyo, suala linalopelekea mishipa ya moyo iwe minene na migumu. Pia huongeza hatari ya kupata mshituko wa moyo, mshituko wa ubongo, figo kutofanya kazi na moyo kushindwa kufanya kazi. Shinikizo la damu linapokuwa pamoja na unene wa kupindukia, uvutaji sigara, kiwango cha juu cha mafuta kwenye damu au kisukari, humfanya mtu apatwe kwa urahisi na mshituko wa moyo.
 Kutoushughulisha mwili: Kuishi maisha yasiyokuwa ya kushughulika kifizikia ni miongoni mwa sababu za kupatwa na ugonjwa wa moyo. Shughuli za kawaida husaidia kuzuia magonjwa ya moyo na kuongezeka kiwango cha mafuta katika damu. Unapoushughulisha mwili wako zaidi ndivyo unavyojisaidia zaidi kiafya. Kushughulisha mwili husaidia kudhibiti kisukari, unene wa kupindukia, kiasi kikubwa cha mafuta katika damu na hata kupunguza shinikizo la damu.
 Unene wa kupindukia au Obesity: Watu wenye unene wa kupindukia wana mafuta mengi mwilini na iwapo mafuta yamejikusanya katika nyonga na kiuno wanaweza kukabiliwa na hatari ya kupata mshituko wa moyo. Unene mkubwa huufanya moyo ufanye kazi zaidi. Pia huongeza shinikizo la damu na kiwango cha mafuta katika damu. Halikadhalika unene humsababisha mtu apatwe na kisukari.
Sababu nyinginezo ni pamoja na
 Mtu kuwa na mawazo na fikra kila mara, kwani wataalamu wanasema kuwa kuna uhusiano kati ya kuwa na mawazo na fikra na magonjwa ya moyo. Kwani mtu mwenye mawazo mengi kwa kawaida huwa na ghadhabu, huenda akavuta sigara na mengineyo ambayo huweza kupelekea ugonjwa wa hatari.
 Kunywa sana pombe: Kunywa sana pombe husababisha shinikizo la damu, magonjwa ya moyo na kupelekea mshituko wa moyo. Pia huongeza kiasi cha mafuta katika damu, kensa na magonjwa mengineyo na hata husababisha moyo kupiga hovyo. Vilevile huchangia katika kusababisha unene wa kupindukia, ulevi wa kupindukia, kujiua na ajali.

No comments: