Monday, November 16, 2009

Kumbuka yafuatayo kabla ya kupaka rangi nywele zako


• Osha nywele zako vizuri kwa shampuu kabla ya kuweka rangi.
• Usiweke kondishena na usitumie shampuu zenye kondishena kwani kondishena itasababishwa rangi isiingie vyema katika nywele.
• Iwapo kichwa chako ni sensitive au nywele zako zimeharibika au kavu, subiri dakika 12 hadi 24 baada ya kuosha ndio upake dawa ya kubadilisha nywele rangi.
• Na wakati unapopaka dawa ya kutia rangi nywele fuata maelekezo vizuri kama yalivyoandikwa.
• Tumia glavu pamoja na taulo, rangi ya nywele inaweza kukuchafua kila mahali, hasa ikiwa katika suala hili wewe si mjuzi.
• Ili kuzuia rangi ya nywele kuingia katika ngozi yako, unaweza kupaka vaselini kuzunguka kichwa, lakini hakikisha haiingia katika nywele kwani inaweza kuingiliana na rangi na kufanya rangi isikole vyema.
• Iwapo rangi itaingia katika ngozi yako, usihofu itaondoka baada ya kuoga mara mbili au tatu. Na wakati unapaka rangi iwapo utaiona imeingia katika ngozi, hapo hapo chukua tishu au karatasi laini na ipake shampuu kidogo na uifute. Itatoka bila matatizo yoyote.
• Tumia kondishena baada ya kuzipaka rangi nywele zako. Ni bora utumie kondishena ambayo ni maalum kwa ajili ya nywele zilizotiwa rangi.

No comments: