Saturday, September 19, 2009

Karoti


Karoti ina umuhimu mkubwa kwa lishe ya mwanadamu. Ikiwa katika umbo la mboga mboga aina ya mzizi, (root vegetable) ina rangi ya machungwa yenye kijani kigogo, inayosababishwa na mada ya Beta carotene, yenye umuhimu katika kutengeneza Vitamin A. Karoti kwanza ina kiasi kukubwa cha ufumwele au fibres, kwa kiasi ambacho katika kila gramu 100 ya karoti, zinapatikana gramu 2 za ufumwele, gramu 240 za Potassium na mikrogiramu 5,330 za Beta-Carotene. Kiasi hicho cha Beta karotini huweza kuufaidisha ubongo kwa zaidi ya kiasi kinachotakiwa. Mada hiyo ya Beta karotine hubadilishwa na mwili na kuwa Vitamin A ambayo ni muhimu sana katika kuimarisha mfumo wa ulinzi wa mwili na ufanyaji kazi mzuri wa ngozi, mapafu na utumbo. Pia husaidia katika ukuaji bora wa seli mwilini. Hivyo watu wenye kusumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu (High Blood Pressure) au wale wanaotaka kupungua uzito na hawataki miili yao ipate nguvu sana kupitia chakula, wanashauriwa kula vyakula vyenye mboga mboga ( vegetables) ikiwemo karoti. Karoti inapunguza kiwango cha mafuta mwilini (cholesterol) na ina Iron, Magnesium, Manganese, Phophorus, na hata Sulphur. Kuna yenyewe ina asilimaia 87 ya maji, vitamin B6, Thiamine, Folic acid na hata Calcium. Ingawa Beta carotene inapatikana katika mboga na matunda mengine lakini hakuna tunda lenye kiasi kikubwa cha mada hiyo zaidi ya karoti. Nukta muhimu ya kuzingatiwa hapa ni kuwa, karoti iliyopikwa inaupa mwili kiasi kingi zaidi cha Beta carotene kuliko karoti mbichi au ambayo haijapikwa.
Jamani shime tule tusisahau karoti katika vyakula vyetu!

No comments: