Monday, November 2, 2009

Kila dakika moja mwanamke anafariki dunia akijifungua


Imetangazwa kuwa idadi ya wanawake wanaofariki dunia wakati wa ujauzito na kujifungua imeongezeka katika nchi nyingi. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mfuko wa Idadi ya watu wa Umoja wa Mataifa (UNFPA), kila dakika moja mwanamke mmoj hufariki dunia wakati wa kujifungua.
Katika mkutano uliofanywa na Mawaziri wa Ulinzi kutoka nchi 150 duniani mjini Addis Ababa Ethiopia, kumeripotiwa kuwa uzazi unasababisha idadi kubwa zaidi ya wanawake wapoteze maisha ikilinganishwa na matukio mengineo kama vile vita. Kutokuwepo wakunga wenye ujuzi wa kutosha, na umbali mkubwa kati ya maeno ya vijijini hadi kwenye vituo vya afya ni miongoni mwa sababu zinazochangia matatizo makubwa na vifo vya wanawake wajawazito. Mawaziri hao wamekubalina kwamba, kuzaa kwa mpango ni moja ya njia za kukabilina na matatizo kama hayo na kwamba, inahitajika serikali ziwekeze zaidi katika elimu ya huduma ya afya.

No comments: