Friday, December 25, 2009

X-Mass Njema Wadau


Leo ni sikukuu ya Christmas, kwanza kabisa blogi ya Kona ya Afya inatoa mkono wa heri na baraka kwa mnasaba wa kuzaliwa masihi, Issa Bin Maryam, (Yesu Kristo) kwa wafuasi wote wa dini hiyo ya mwenyezi Mungu. Ni matumaini yetu kuwa katika wakati huu wa sikukuu ya X-mass wadau wote huku wakisherekea sikukuu na kuwa mapumzikoni, hawatazembea pia kuzitunza afya zao. Kwa ajili hiyo basi zifuatazo ni nukta kadhaa za kufuata ili kuepusha wasiwasi na mfadhaiko wa mawazo (stress) wakati huu wa mapunziko na sikukuu, na zinazosadia kuhakikisha kwamba tunabaki katika afya njema kimwili, kiakili na kihisia.
• Jitahidi kushikamana na ibada. Kushikamama na ibada za kiroho wakati huu wote wa sikukuu, na kuwa karibu na muumba ( kwa kutegemea imani na dini ya mtu) kwa kufanya ibada kama kusali, kwenda kanisani au msikitini husaidia kumfanya mtu ajisikie vizuri kiroho.
• Pata hewa nzuri. Kila unavyojitahidi kuwa nje ya nyumba na kufanya shughuli mbalimbali ndivyo mwili wako unavyopata nishati zaidi. Kuvuta hewa safi na salama kutaufanya ubongo wako upate oksijeni zaidi na kuupa mwili wako nishati. Hivyo wakati huu wa sikukuu jitahidi kufanya michezo kama vile kukimbia, kusketi, kupanda baiskeli, kutembea kando ya bahari au mto na kadhalika.
• Jishughulishe na masuala ya sikukuu kama vile kuwanunualia watu zawadi madukani, kuwatembela ndugu jamaa na marafiki na hata wagonjwa, kualika au kwenda katika mialiko mbalimbali na kadhalika. Vitendo hivyo ni bora kuliko kukaa tuu nyumbani na kula na kunywa peke yako huku akiangalia tv au filamu.
• Pata usingizi wa kutosha na pumzisha mwili wako. Unaweza ukalala kidogo mchana au kuamka kwa kushelewa kidogo wakati wa asubuhi.
• Tenda kile moyo wako inachopenda. Kuwa na afya njema wakati wa X-mass ni pamoja na kufanya kile kinachoburudisha moyo wako. Imba kama unapenda kuimba, cheza kama unapenda kucheza, andika, tembea, chora picha, pika nakadhalika, ilimradi utende chchote kili kinachofaurahisha moho wako.
• Kula na kunya kusizidi kiasi, na bila kusahau vyakula visivyo na mafuta mengi au sukari nyingi ambavyo ni salama kwa afya zetu. Wale wenye magonjwa mbalimbali sugu wasijisahau na kuvunja miiko ya vyakula wasivyotakiwa kula. Usisahau kuwa, sikukuu itapita lakini afya yako ni muhimu sana kwa maisha yako yote… Sikukuu njema wadau huku tukitunza afya zetu!

No comments: