
MTAALAMU wa masuala ya uzazi wa mpango, wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Calista Simbakalia, amesema vidonge vya uzazi wa mpango havileti saratani ya uzazi kama inavyodaiwa na baadhi ya watu.
Simbakalia alitoa kauli hiyo juzi jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa mada katika semina ya kutambulisha uzinduzi wa mpango mkakati wa uzazi wa mpango utakaofanyika Machi 30, chini ya wizara hiyo kitengo cha Uzazi wa Mpango na Mtoto.
Alisema si kweli kuwa vidonge vya uzazi wa mpango husababisha ugonjwa wa saratani ya uzazi bali vidonge hivyo hutumika pia kwa matibabu ya ugonjwa huo.
“Kumekuwa na kundi kubwa la watu ambao wamekuwa wakiamini matumizi ya dawa hizo huleta saratani ya uzazi wakati ukweli ni kwamba zimekuwa zikisaidia kutibu ugonjwa huo.”
Simbakalia alisema kuwa mwanamke asiyetumia njia za uzazi wa mpango hubeba mimba kila wakati jambo linalomfanya muda mwingi autumie katika kulea watoto badala ya kufanya shughuli za uzalishaji mali.
Alibainisha kuwa ubebaji mimba wa mara kwa mara humfanya mwanamke kuwa tegemezi sambamba na kuifanya familia husika kutopiga hatua za maendeleo.
“Mama atakapotumia uzazi wa mpango unamsaidia kutopata mimba ambayo hakuipanga; hivyo atatumia muda wake mwingi kufanya shughuli za kumuongezea kipato,” alisema.
Naye mratibu wa taifa wa shughuli za uzazi wa mpango nchini, Maurice Hiza, alisema uzazi wa mpango unasaidia kupunguza vifo kwa kina mama wajawazito sambamba na kuboresha afya ya mama na mtoto wake.
Alibainisha kuwa uzazi wa mpango pia huisaidia serikali kuboresha huduma za jamii kama elimu, miundombinu, huduma za afya ambazo zimekuwa zikilegalega kutokana na uwiano mdogo kati ya idadi ya watu na uwezo wa serikali.
Alisema wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wamepanga kuwaelimisha wanaume ambao inadaiwa ndiyo kikwazo kikubwa cha kuwakubalia wake zao au wao wenyewe kutumia njia zinazotakiwa za uzazi wa mpango.
Aliongeza kuwa iwapo elimu ya uzazi wa mpango itayafikia makundi ya vijana wanaochipukia na wanaume wakaelewa dira ya taifa ya mpango mkakati wa kupunguza vifo vya kina mama hadi kufikia mwaka 2010 -2015 itafanikiwa kirahisi.
1 comment:
Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.
Mume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.
Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na akafanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
Nitaendelea kushukuru milele.
Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi wa kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
. Usaidizi wa kurejesha ndoa
. Tamaduni za ujauzito za kupata mimba
. Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
. Mwongozo na ulinzi wa kiroho
Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159. dawnacuna314@gmail.com
Post a Comment