Monday, March 15, 2010

Kensa zinazoshambulia kizazi … sehemu ya kwanza


Kuna kensa mbalimali tofauti zinazoweza kushambulia sehemu mbalimbali za kizazi na mfuko wa uzazi. Lakini kensa ambayo inajulikana sana pengine kutokana na kuwepo vipimo vya kujua kama kensa hiyo ipo au la ni kensa ya mlango wa uzazi (cervical cencer) ambayo hushambulia mdomo au shingo ya kizazi. Kensa hiyo huweza kugunduliwa mapema na kwa urahisi baada ya wanawake kufanyiwa kipimo cha kupima kensa hiyo na pale inapoonekana kuna mabadiliko yasiyo ya kawaida katika seli za kizazi ambazo mwanzoni huwa bado hasijageuka kuwa kensa kamili. Mabadiliko ya mwanzo ya seli hizo kuelekea kwenye saratani huwa ni rahisi kutubiwa, suala ambalo limepelekea idadi ya wanawake wanaosumbuliwa na ugonjwa huo ipungue katika miaka ya hivi karibuni. Kensa nyingine inayowatokea sana wanawake ni kensa ya kizazi (uterine cancer) au kensa inayoshambulia mji wa mimba. Kensa hiyo hushambulia kuta za kizazi. Kensa ya kizazi kwa hakika ni kensa inayoshambulia mwili wa kizazi ambao umejengwa kwa tishu mbalimbai kutoka katika mlango wa uzazi hadi ndani ya kizazi chenyewe. Kensa ya kizazi mara nyingi huwapata wanawake wenye umri mkubwa ambao hedhi yao imeshakatika, na mara nyingi hushauriwa waondolewa kizazi. Wataalamu wanasema kwamba, suala muhimu linaloweza kufanikisha matibabu ya kensa ya mlango wa uzazi na ya kizazi ni kugunduliwa mapema magonjwa hayo. Kensa nyingine ambayo haishuhudiwi sana ni kensa inayoshambulia kizazi iitwayo Uterine Sarcoma, ambayo hushambulia misuli ya kizazi. Kensa hiyo hufananishwa zaidi na saratani nyinginezo zinazoshambulia misuli kuliko saratani za kizazi.
Si vibaya kujua yafuatayo kuhusiana na ugonjwa wa kensa:
Kensa ya matiti ndio kensa inayotokea zaidi duniani huku kensa ya korodani ikiwa inatokea kwa chache zaidi.
Hii ni katika hali ambayo kensa inayoongoza kwa kusababisha vifo vingi zaidi vya wanawake ni kesna ya kensa matiti huku kensa ya mapafu ikishika namba ya kwanza kwa kupelekea wanaume kufa kwa wingi.
Kati ya watu watatu mmoja anatabiriwa kupata kensa nchini Uingereza kwenye miaka ijayo.
Kensa ya matiti inaongezeka huku kensa ya mapafu ikitarajiwa kupungua kutokana na kupungua wafutaji sigara.
Usikose kufuatilia zaidi makala zijazo zinatakazojadili kensa mbalimbali.
Daima na tutunze afya zetu!

No comments: