Wednesday, March 3, 2010

Mama wajawazito wenye kuongezeka uzito sana wana hatari ya kupata kisukari cha mimba


Kina mama wenye mimba ambao huongezeka uzito kwa kasi katika miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito wanakabiliwa na hatari ya kupata kisukari cha mimba (gestational diabetes). Kifafa cha mimba ni hali ambayo wanawake ambao huko nyuma hawakuwa na ugonjwa wa kisukari huonekana kuwa na ongezeko la sukari katika damu kwa mara ya kwanza wakati wa ujauzito. Kwa mujibu wa uchunguzi mpya, mama wajawazito ambao wataongeza uzito wa gramu 403.70 kwa wiki wako katika hatari ya kupata kisukari cha ujauzito zaidi ikilinanishwa na wale watakaoongeza uzito wa chini ya gramu 272.15 kwa wiki. Bi. Monique Hedderson aliyeongoza uchunguzi huo amesema kuwa, ongezeko kubwa la mafuta ya mama mwanzoni mwa mimba kunaweza kukaathiri kwa kiasi kikubwa tishu za mwili na kuzifanya zisikubali insulin, jambo ambalo taratibu husababisha kisukari cha ujauzito. Kwa ajili hiyo wataalamu wameshauri kwamba, wakina mama wenye mimba hasa wale wanene na wenye uzito mkubwa wanapaswa wajiepushe na kuongezeka uzito mwanzoni mwa mimba ili wasipwatwe na kisukari cha mimba.
Sio vibaya kutambua kwamba, asilimia 4 ya kina mama ambao watapata kisukari wakati wa ujauzito wanakabiliwa na hatari ya kupata ugonjwa wa kisukari baadaye maishani mwao, hiyo ikiwa ni pamoja na watoto wao. Kisukari cha ujauzito kina dalili kadhaa lakini kwa kawaida huainishwa kwa vipimo (screening) vinavyochukuliwa wakati wa ujauzito.

No comments: