
Kufanya mazoezi wakati wa ujauzito kuna umuhimu mkubwa kwa afya ya mama mjamzito mwenyewe na mtoto wake ambaye bado hajazaliwa. Wanawake wengi wanatambua umuhimu wa kula lishe bora, kuhudhuria kliniki, kuacha kuvuta sigara na kunywa pombe wakati wakiwa na mimba. Lakini si wanawake wengi wanaoelewa umuhimu wa kutumia muda wao kufanya mazoezi wakati wa ujauzito. Mazoezi yana umuhimu mkubwa kiafya wakati wa ujauzito kama ilivyo kabla ya ujauzito. Kufanya mazoezi wakati unapobeba mimba kunaleta faida kubwa wakati wa kujifungua. Wakati wa ujauzito ni muhimu kudhibiti ongezeko la uzito wa mama. Kwa kujishughulisha mama mjamzito na kuwa na harakati humsaidia awe na afya bora na kumsaidia aweze kupitisha kipindi cha uchungu na kujifungua kwa urahisi zaidi. Zaidi ya kumsaidia mama asiongeze uzito mkubwa wakati wa mimba, kufanya mazoezi humsaidia mama pia kurejea katika uzito wake wa kawaida kwa urahisi baada ya kujifungua kwa kawaida au kwa uparesheni. Kwa ujumla mama mjamzito kama ambayo anavyoshauri kula chakula bora na kuwa na afya nzuri wakati wa ujauzito, hivyo hivyo hushauriwa pia kuzingatia suala zima la kufanya mazoezi na kuchunga mwili wake usiongeze uzito mkubwa. Pia kufanya mazoezi huufanya mwili utoe mada ya endorphins, ambayo husaidia kumfanya mama asipate matatizo ya kifikra na msongamano wa mawazo (emotional stress na depression).
Zifuatazo ni faida anazozipata mama mjamzito iwapo atafanya mazoezi
1. Mazoezi hupunguza maumivu ya kichwa, kukosa choo na kuvimba mwili.
2. Mazoezi huongeza nguvu na kuupa mwili stamina.
3. Mazoezi hukufanya ujisikie vizuri na kukufanya uwe katika hali ya furaha.
4. Mazoezi hupunguza maumivu ya mgongo na huimarisha mifupa ya mgongo, makalio na mapaja na kuifanya iwe na uwezo wa kuvumulia vyema uzito wa mimba.
5. Mazoezi husaidia huongeza mtiririko wa damu na hewa katika ngozi na kuifanya ngozi yako ionekane nzuri.
6. Mazoezi hutayarisha mwili wako uwe tayari kwa ajili ya kuhisi uchungu kwa muda mfupi na kujifungua kwa urahisi.
7. Mazoezi hufanya mwili wako urudi upesi katika muonekano wake wa kawaida baada ya kujifungua.
8. Mazoezi humsaidia mama mjamzito apate usingizi kwa wepesi na kulala vyema.
Hata hivyo mama majamzito anashauriwa kabla ya kuanza kufanya mazoezi apate ushauri wa daktari na kuhakikisha kuwa hana matatizo ambayo kwa kufanya mazoezi pengine yakahatarisha mimba yake. Kwa wale waliokuwa wakifanya mazoezi kabla ya kubeba mimba wanashauriwa kuendelea na mazoezi yao lakini kwa kuwa waangalifu na kwa kiwango kidogo. Lakini kwa wale ambao walikuwa hawafanyi mazoezi hawaruhusiwi kufanya aina zote za mazoezi wakati wa ujauzito. Mazoezi kama vile kuogelea (kwa wale anaojua kuogelea), kutembea na yoga ni miongoni mwa mazoezi yanayoshauriwa wakati wa ujauzito. La muhimu ni mama mjamzito kutokaa tu na kujiepusha na uvivu na pengine kwa kufanya shughuli zake tu za kawaida ambazo mama huwa anazifanya nyumbani kila siku ikawa inatosha kuwa mazoezi yake na akaongeza kwa kutembea kidogo ( walking) kila jioni. Kutembea ni mazoezi salama na rahisi kwa kila mama mjamzito na yanayojulikana na kila mtu na kuweza kufanywa mahala popote. Ni bora kama unaweza fanya mazoezi na mwenza wako, rafiki au hata ndugu na jamaa yako ili uweze kufurahia zaidi mazoezi hayo. La muhimu ni kufuata maelekezo ya daktari kwani si kila mama mjamzito anaruhusiwa kufanya mazoezi wakati wa ujauzito kutokana na sababu tofauti. Baadhi ya mazoezi ambayo yana madhara kwa afya ya mama mjamzito na kwa mtoto hayaruhusiwi kabisa kufanywa wakati wa ujauzito. Mazoezi hayo ni kama vile mazoezi ya aerobic, ski, kupanda mawe, kupanda farasi na mengineyo kama hayo. Iwapo unaishi katika miji iliyoendelea basi unaweza kupata kwa urahisi vituo maalum kwa ajili ya kufanyia mazoezi mama wajawazito, na katika vituo hivyo kwa kawaida wakina mama wajawazito hukusanyika na kufanya mazoezi kwa pamoja. Lakini kama uko katika miji ambayo vituo hivyo hakuna usife moyo, na jitahidi kufanya mazoezi hayo peke yako huku ukishirikiana na familia yako.
Makala hii inaendelea...
4 comments:
Asante kwa Makala yako nzuri.
Sawa nitakujulisha Mwenzi wangu kwani ni Mjamzito
Sawa nitamjulisha Mwenzi wangu kwani ni Mjamzito
Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.
Mume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.
Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na akafanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
Nitaendelea kushukuru milele.
Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi wa kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
. Usaidizi wa kurejesha ndoa
. Tamaduni za ujauzito za kupata mimba
. Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
. Mwongozo na ulinzi wa kiroho
Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159. dawnacuna314@gmail.com
Post a Comment