Tuesday, March 30, 2010

Mama mjamzito pia anatakiwa kuzingatia dalili zifuatazo wakati anapofanya mazoezi, na anashauriwa kuacha haraka kufanya mazoezi anapohisi kuwa na dalili hizo:
• Kutoka damu ukeni.
• Kuhisi kizunguzungu au kuzimia, au kukosa nguvu.
• Kukosa pumzi au pumzi kumbana.
• Maumivu ya kichwa.
• Maumivu ya kifua.
• Misuli kukosa nguvu.
• Miguu kuuma na kuvimba.
• Maimivu ya mgongo na kiuno.
• Kujisikia uchungu au dalili za kujifungua kabla ya muda.
• Kupungua harakati ya mtoto ( kupungua hali ya kupiga mtoto tumboni)

No comments: